HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, May 10, 2018

YALIYOJIRI BUNGENI LEO JIJINI DODOMA

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama akimsikiliza Mbunge wa Songea Mjini Mhe Dkt  Damas Ndumbaro wakati wa kikao cha ishirini na sita cha mkutano wa kumi na Moja leo Jijini Dodoma.
 Waziri Mkuu, Mhe.Kassim Majaliwa akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri mkuu Bungeni leo Jijini Dodoma. 
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Job Ndugai akiongoza kikao cha ishirini na sita cha mkutano wa kumi na Moja leo Jijini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Nishati Mhe.Subira Mgalu akitolea ufafanuzi masuala mbalimbali ya Nishati wakati wa kikao cha ishirini na sita cha mkutano wa kumi na Moja leo Jijini Dodoma.
 Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akizungumza jambo na Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Harrison Mwakyembe wakati wa kikao cha ishirini na sita cha mkutano wa kumi na Moja leo Jijini Dodoma.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe.Charles Mwijage akionyesha kitabu chenye idadi ya Viwanda vyote nchini wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2018/2019.Kitabu hicho kina kurasa mia tisa.
 Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo  Mhe.Dk.Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Sumve Mhe.Richard Ndassa  wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati ya maudhui ya mamlaka ya mawasiliano Tanzania(TCRA)  walipomtembelea leo Bungeni.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo  Mhe.Dk.Harrison Mwakyembe akimskiliza Mbunge wa Sumve Mhe.Richard Ndassa Bungeni leo Jijini Dar es Salaam.
Picha zote na Daudi Manongi,MAELEZO,DODOMA

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad