HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, October 29, 2015

VODACOM YAWATUNUKU ZAWADI MBALIMBALI WASHIRIKA WENZA WA KIBIASHARA.

 Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania, Keith Tukei(kushoto)akimkabidhi Bw.Ajali Kibiki(kulia)cheti cha utendaji bora wa kutoa huduma  nzuri  kwa wateja  katika duka la kampuni hiyo lililopo Makamba Mkoani Njombe,Wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa na kampuni hiyo kwa ajili ya kutoa elimu kwa  washirika wa kibiashiara.Wengine katika picha wapili toka kushoto ni Magreth Lawrence na Brigita Stephen.Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
Mshirika wa kibiashara wa Vodacom Tanzania,Moshi Kimila mkazi wa Kasulu mkoani kigoma(kulia) akifurahia kwa kupata tuzo ya utendaji bora wa kazi aliyokabidhiwa na Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa kampuni hiyo, Keith Tukei(kushoto) Wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa na kampuni hiyo kwa ajili ya kutoa elimu kwa  washirika wa kibiashiara na kuwatunuku tuzo na vyeti  mbalimbali kwa watendaji bora. Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. 
 Mkuu wa kitengo cha huduma  za kifedha wa Vodacom Tanzania, Evans Lyimo(kulia) akiongea na baadhi ya washiriki katika  warsha ya kutoa elimu kwa  washirika wa kibiashiara iliyoandaliwa  na kampuni hiyo kwa ajili ya kuweza  kuendelea kuboresha huduma za kibiashara katika jamii. Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
 Mshirika wa kibiashara wa Vodacom Tanzania,Lilian Minja  mkazi wa jijini Dar es salaam(kulia) akifurahia kwa kupata cheti cha utendaji bora wa kutoa huduma   kwa wateja  alichokabidhiwa na Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa kampuni hiyo, Keith Tukei(kushoto) Wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa na kampuni hiyo kwa ajili ya kutoa elimu kwa  washirika wa kibiashiara na kuwatunuku tuzo na vyeti  mbalimbali kwa watendaji bora,katikati ni Andrew Temu. Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad