libeneke hili sikuzote na kama kawaida huwa haliwi mbali na mitaa, katika katiza katiza mtaani leo ikakumbuna na tukio la mweleka wa bodaboda katika eneo la mwanjelwa mtaa wa kongo jijini mbeya, chanzo cha mweleka huo ni kama kawaida yao bodaboda na haraka zao katika harakati za kumkwepa muungwana alie kuwa akikatiza mdogo mdogo.
jamaa wa pikipiki wakiicheki pikipiki yao kama iko vizuri kabla ya kujicheki wao kwanza huku wakipewa semina ya nguvu kutoka kwa wafanya biashara wa eneo hilo.
No comments:
Post a Comment