HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, July 2, 2014

Bonnah Education Trust Fund kuwasomesha sekondari wanafunzi 100

Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Elimu wa Bonnah (Bonnah Education Trust Fund), Bonnah Kaluwa (katikati) akizungumzia uzinduzi wa Awamu ya Pili ya Mpango wa ‘Elimu Mwanzo Mwisho’, ambapo wanafunzi wengine 100 wasio na uwezo na yatima wa jijini Dar es Salaam watakaofaulu kujiunga na elimu ya sekondari watanufaika na mpango huo kwa kulipiwa ada.Mfuko huo umeandaa Chakula cha Hisani Agosti mwaka huu.
Meneja Mkazi wa Kampuni ya Resolution Health, Oscar Osula (kulia) akielezea kampuni hiyo kuwa moja ya wadhamini wa mpango huo wa kuwawezesha watoto wasio na uwezo na yatima kupata elimu ya sekondari.
Meneja Rasilimali Watu na Utawala wa Kampuni ya Aramex Tanzania Limited, Jane Njagi (kushoto) akizungumzia namna kampuni yake ilivyoamua kuwaunga mkono Bonnah Education Trust Fund kwa kuwadhamini kuhakikisha watoto 100 wanapata ada za elimu ya sekondari.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad