HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, April 30, 2013

TAASISI YA KIJAMII YA FOWARD MOTION ikishirikiana na Doctor's Plaza Heart Clinic pamoja na Lancet Laboratories yazindua kampeni ya kupima afya

FOWARD MOTION ikishirikiana na Dorctor's Plaza Heart Clinic pamoja na Lancet Laboratories wamezindua mpango wa  upimaji afya (Medical checkup) mwishoni mwa juma katika makao makuu ya  Doctor's Plaza Heart Clinic yaliyopo Sea View jijini Dar es salaam. 

Katika siku hii  washirika hao walitoa huduma ya bure ya upimaji wa Cholestrol, Sugar, Blood Pressure, ECG na BMI. Waalikwa wote walipata fursa ya kupima vipimo hivyo na kupata ushauri wa bure (free consultation) kutoka kwa madaktari Bingwa Campaign hiyo pia iliambnatana na mafunzo mbalimbali ya afya kutoka kwa mabingwa hao.

Kwa mujibu wa msemaji wa DPHC, Bi Sofia Byanaku,  Mpango huo endelevu, utaendelezwa kwa njia tofauti na ngazi tofauti, akisisitiza kuwa Kinga ni bora kuliko Tiba!
 Wadau wakisikiliza maelezo toka kwa madaktari kuhusu umuhimu wa kupima afya
 Dkt Masatu akitoa elimu ya bure kuhusu umuhimu wa watu kupima afya zao
Dkt Vivian mlawi akitoa ushauri kwa Nancy Sumary aliyekuwa mmoja wa wadau waliofika kupata huduma hiyo ya bure ya kupimwa afya na kupewa ushauri

 wadau wakisubiri zamu kupimwa
Nesi akimpima bloga maarufu Missie Popular
  Doctor's Plaza Heart Clinic ilihudumia wadau kibao siku hii
 Wafanyakazi wa  Doctor's Plaza Heart Clinic wakijadiliana namna ya kuendesha kazi siku hii
  Mama akijiandikisha Doctor's Plaza Heart Clinic
 Kumbukumbu zinawekwa kwa uangalifu

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad