Bondia Japhert Kaseba (kulia) akimwaga wino kwenye katarasi ya mkataba wa kucheza na Francis Cheka siku ya sabasaba,jijini Dar es Salaam.kushoto ni Mdau Khalifa Kiumbemoto.
Na Mwandishi Wetu
BINGWA wa kick Boxing nchini, Japhet Kaseba leo amesaini mkataba wa kucheza na Bingwa
wa dunia wa ndondi mwenye mkanda unaomilikiwa na IBC, Francis Cheka wa
Morogoro katika uzani wa KG 75 utakaofanyika siku ya sabasaba jijini
Dar es Salaam
Akizungumza wakati wa kusaini mkataba huo Kaseba
amesema anashukulu kupata mpambano huo na atahakikisha anaonyesha uwezo
wake wote katika mchezo huo kwani yeye ni bingwa wa mapambano
"Najua
mabondia wa hapa bongo wananikwepa sana kwa kuwa nimeshakuwa bingwa wa
ngumi za mateke lakini awajui mimi ni bingwa katika mapigano yote"
alisema Kaseba
Kaseba aliendelea kusema "Nitahakikisha naweka kambi ya kutosha na
kukata ngebe za cheka ni mtoto mdogo sana katika masumbwi kwa kweli
bingwa wa kweli ni Rashidi Matumla ambaye ninamuheshimu mpaka sasa cheka
kanikimbia muda mrefu tu tangia tupambane 3 October 2009 ambapo alipewa
ubingwa kwa kusingizia mshabiki wangu alikuja kumtupa nje ya uwanja
kazi yake yeye anarudiana na Mada Maugo kila siku lakini kwa sasa
kakanyaga miwaya zamu yake imefika"
Nae Promota wa mpambano huo
Kaike Siraju amesema mpambano huo utakaofanyika Dar es salaam siku ya
sabasaba utakuwa ni mpambano ambao aujawai kutokea kwa kuwa mabondia hao
wanakubalika na mashabiki wa ndani na nje ya Nchi
Mbali na mpambano huo pia kutakua na mapambano ya utangulizi na burudani mbalimbali ambazo mtatangaziwa baadae
No comments:
Post a Comment