HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, March 24, 2012

Vilio vyatawala katika zoezi la bomoabomoa katika nyumba zilizokuwa za watumishi wa Mamlaka ya Bandari na Reli mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam ili kupisha ujenzi wa kituo cha mabasi yaendayo kasi

Wakina Mama na Watoto zao wakiwa wamekaa chini bila kujua la kufanya wakati zoezi la kubomoa nyumba walizokuwa waliishi za Mamlaka ya Bandari na Reli mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam ili kupisha ujenzi wa kituo cha mabasi yaendayo kasi likiendelea.
Mtoto akiwa amelala kwenye godoro lililokuwa limetolewa nje na vyombo vingine ili kupisha zoezi la bomoa bomoa nyuma ambazo zilikuwa zikitumiwa na watumishi wa Mamlaka ya Bandari na Reli mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam ili kupisha ujenzi wa kituo cha mabasi yaendayo kasi
Bati ziking'olewa.
Wazee wa kazi pia walitia timu eneo la tukio.
Mawasiliano ya ndugu na jamaa yakiendelea huku wengine huzuni zikiwa zimewatawala usoni mwao.
Greda likiwajibika.

(Picha na Francis Dande)

1 comment:

  1. ipo sehemu wamepangiwa kuenda kuishi au ndo kibongobongo watajiju,sio fiti kabisa especially wen kids are involved waende wakakae na takaya ikulu vyumba kibao.

    ReplyDelete

Post Bottom Ad