ASSALAM ALYIKUM WARAHMATU ALLAHI
Hakika moja ya neema tuliyoipata sisi ni kuwa Waislamu na kupata Mtume Muhammad (S.A.W) kuwa ni rehma kwetu na kigezo chema kwetu...
Mwenyezi Mungu anasema katika kitabu chake kitukufu suratul-Ahzab aya ya 15:
Bila shaka mnao mfano mwema (ruwaza nzuri) kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, kwa mwenye kumuogopa Mwenyezi Mungu na siku ya Mwisho na kumtaja Mwenyezi Mungu sana.
Kutokana na mnasaba wa mwenzi huu wa mfungo sita Madrasatul Al-Amin iliyokuwepo katika mji wa Toronto inafuraha kuwaalika ndugu zetu nyote katika Maulid ya Mtume Muhammad. Yatakayofanyika katika anuani ifuatayo:
LAWRENCE HEIGHTS COMMUNITY CENTRE
REPLIN RD TORONTO ONTARIO M6A-2M8
PHONE NUMBER 416 395 6118
Maulidi pamoja na kuonyesha kile wanachokipata wanafunzi kwa Walimu wao kwa upande wa masomo. Maulidi yataongonzwa na Ust Abdullah Abubakar Mtawa pamoja na wanafunzi wa Madrasatul Al-Amin Toronto.
Maulidi ya takuwa mnamo tarehe 18 Feb 2012 saa 2:30.Kuhudhuria kwenu ndio mafanikio yetu kwa maelezo zaidi waweza kupiga simu namba:647 994 3028 au 647 774 1133. Ni matumaini yetu tuta jumuika pamoja katika kusherehekea mazazi ya Mtume wetu Muhammad (S.A.W).
Imetolewa na Al-Amin.
No comments:
Post a Comment