Kampuni ya African Stars Entertainment imeandaa tamasha kubwa la burudani kwa jili ya kusherehekea miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara na Uzinduzi rasmi wa Albamu ya 11 ya Bendi yake ya African Stars "Twanga Pepeta".
Tamasha hilo linataraji kuwahusisha wasanii wa fani mbalimbali za Muziki wa hapa nchini na kutoka nje ya nchi. Fani zitakazohusishwa ni pamoja na Taarab, Muziki wa Kizazi kipya na Muziki wa Dansi na msanii mmoja kutoka Nchini Kenya ambaye bado uongozi wa ASET unaendelea kufanya naye mazungumzo.
Tamasha hilo la uzinduzi linataraji kufanyika katika viwanja vya Leaders Club vilivyopo maeneo ya Kinondoni Jijini Dar es salaam siku ya Jumapili ya tarehe 06-11-2011 kuanzia saa sita za mchana.
Nyimbo zote zimesharekodiwa katika CD kwenye studio ya Metro chini ya Mtengenezaji Allen Mapigo na nyimbo tatu zinatamba redioni na kwenye stesheni za redio mbalimbali hapa Nchini na nje ya nchi.
Maandalizi ya Tamasha yanaendelea vizuri na katika kufanikisha Tamasha hili, ASET imeandaa ligi ndogo itakayoshirikisha timu 12 ikiwemo Timu ya Twanga Pepeta FC iliyoundwa na wanamuziki na wadau wa karibu wa Bendi.
Uzinduzi wa mwaka huu tumeamua kuuweka tofauti kama zinduzi zilizopita ili kuenda sambamba na maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania Bara. Bendi inataraji kuingia kambini wiki moja kabla ya tarehe ya uzinduzi ili kujitayarisha vizuri kwa ajili ya shoo kali.
No comments:
Post a Comment