Bryan Robson |
Mc hezaji nyota wa zamani wa Klabu
ya Manchester United na timu ya Taifa ya Uingereza Bryan Robson anatarajiwa
kuwasili nchini kesho kwa ajili ya kufungua kliniki ya Kimataifa ya
Airtel Rising Stars itakayofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kliniki hiyo itaanza
Jumapili, Oktoba 30 chini ya makocha wa Klabu ya Manchester United ambao
ni Mark Fagan, Paul Bright na Billy Miller na kuhudhuriwa na washiriki
kutoka nchi za Kenya, Malawi, Sierra Leone na Tanzania.
Kliniki hiyo itakuwa
ni hitimisho ya michuano ya Airtel Rising Stars 2011 ambayo ilizinduliwa
mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu na mshambuliaji wa zamani wa Manchester
United Andrew Cole, ambaye aliitumikia Klabu yake hiyo kwa misimu saba
na kuisaidia kutwaa mataji matano kati ya 19 ambayo Manchester United
imeyanyakua hadi sasa.
Airtel Rising Stars ni
mpango kambambe wa kutafuta vipaji chipukizi vya soka kutoka ngazi ya
chini hadi Taifa. Airtel Rising Stars ilishirikisha shule za sekondari
24 mwaka huu kutoka mikoa ya Mwanza, Iringa, Morogoro na Dar es Salaam
ambapo washiriki walionyesha uwezo mkubwa wa soka na hasa katika fainali
zake ambazo zilichezwa katika Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam.
Akizungumzia juu ya michuano
hiyo, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini, Leodger Tenga alisema,’
Huu ni mpango muhimu sana kwa maendeleo ya mpira wa miguu hapa Tanzania.
Na kile ambacho kinafanya Airtel Rising Stars kuwa muhimu zaidi ni ule
ushirikiano wa kampuni hiyo na Manchester United, ambayo ni moja ya
Klabu kubwa duniani. Hii inaifanya kuwa moja ya kitu kikubwa kutokea
katika soka la Tanzania. Tunayofuraha kuwa kwenye ushirikiano huu na
tunahaidi ushirikiano wetu zaidi ya hapo’.
Airtel inayofuraha kujihusisha
na soka ambayo imekuwa ikiwaunganisha pamoja jamii pamoja na kuwafanya
wachezaji kupata mbinu za soka ambazo zitawezesha waweze kuishi kwa
kutegemea soka kama ajira.
Kliniki hii itawapa fursa
vijana kupata mbinu mpya za soka chini ya wakufunzi bora zaidi na kuwafanya
kuongeza uwezo zaidi.
Programu ya Airtel Rising
Stars ni mpango wa Afrika nzima wenye lengo la kuwajengea mawakala,
makocha, mamlaka za soka na wadau wengine fursa ya kuona vipaji vya
wanasoka chipukizi na kutumia nafasi hiyo kuviendeleza ili kupata wachezaji
wazuri kwa faida ya taifa.
No comments:
Post a Comment