HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, September 11, 2011

SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA WALIOPATA AJALI YA MELI ZANZIBAR TOKA CHUO KIKUU CHA KIMATAIFA CHA KIMAREKANI (USIU); NAIROBI, KENYA


Jumuiya ya wanafunzi Watanzania wanaosoma katika Chuo Kikuu cha kimataifa cha Kimarekani (USIU) jijini Nairobi; Nchini Kenya imepokea kwa simanzi zito na masikitiko makubwa habari ya kuzama kwa meli ya MV Spice Islander Alfajiri ya tarehe 10 Septemba, 2011 ikiwa safarini kutokea Kisiwani Pemba kuelekea Kisiwani Unguja. Hakika ni janga zito kwa Taifa letu kwa ujumla.

Jumuiya ya wanafunzi Watanzania wanaosoma katika Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kimarekani (USIU) jijini Nairobi nchini Kenya inapenda kuwasilisha salamu zetu za dhati kabisa za rambirambi kwa Mheshimiwa Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dr. Ali Mohammed Shein, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Viongozi wote wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Wazanzibar na Watanzania wote kwa ujumla, Ndugu zetu wote waliopoteza Ndugu, Jamaa, Rafiki, Mzazi, Mwenza na kadhalika. Tunamuomba Mola atupe Moyo wa Ustahimilivu na Imani ya kuweza kupita katika kipindi hiki kigumu kwetu sote.

Tunamuomba Mola aliye mwingi wa rehema awalaze Ndugu zetu mahala pema peponi. Pia, tunawaombea majeruhi wote wa ajali hii ya kusikitisha waweze pona haraka na kurejea katika shughuli za kujenga taifa. Amin.

Inna Lillahi wa Inna Illahi Rajuun.

Glen S. Kapya
Mwenyekiti
Jumuiya ya Watanzania
Chuo cha Kimataifa cha Kimarekani (USIU)- Afrika

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad