Never say never with ATCL
Kaimu Mkurugenzi Mkuu Bw. Paul Chizi (mwenye suti) akiipokea ndege hiyo
Ndege ya aina ya Dash 8-300 ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) iliyokuwa nchini Afrika Kusini kwa muda mrefu kwa matengenezo imerudi nchini juzi jumamosi jioni tayari kuanza kazi.
Ndege
hiyo iliyokuwa inaendeshwa na Kapteni Pandya na Kapteni Lila iliwasili
kwenye Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere saa 12.45 jioni na
kupokewa na wafanyakzai wa ATCL wakiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu Bw.
Paul Chizi.
Akiongea na vyombo vya habari uwanjani hapo Bw. Chizi alisema Shirika lake linajipanga
kumaliza taratibu muhimu kabla ya kuanza tena safari zake. Alisema
iwapo mambo yote yatakuwa yamekamilika kufikia tarehe 25 Septemba mwaka
huu, ndege hiyo itaanza safari za kwenda moja kwa moja Kigoma kila siku.
Aliongeza kuwa baada ya muda
mfupi, wataanza safari za kwenda Tabora mara nne kwa wiki. Bw. Chizi
ambaye ameteuliwa hivi majuzi kuongoza ATCL alisema baada ya mwezi mmoja
wataanza safari za kwenda Zanzibar na Arusha.
Kuhusu
kuongeza idadi ya ndege, Bw. Chizi alisema kuna Dash 8-300 nyingine
ambayo itafanyiwa matengenezo hapa hapa nchini hivi karibuni ili kuokoa
pesa na muda. Hata hivyo alifafanua kuwa tayari wameweka mkataba na
kampuni ya Jetlink (T) Ltd wa kupata ndege nyingine haraka iwezekanvyo
endapo kutakuwa na haja hiyo.
Bw. Chizi aliongeza kuwa ATCL
ina mipango ya muda mrefu ya kununua ndege zingine mbili za aina ya CRJ
700 zenye uwezo wa kubeba watu 70 ili kuzidi kuonggeza ubora wa huduma
zake.
No comments:
Post a Comment