Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Chai Tanzania, Anne Makinda, ambaye ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,akifafanua jambo katika hotuba yake ya kumkaribisha Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Jumanne Maghembe ( hayupo pichani) kufungua mkutano wa wadau wa chai mwaka 2011.

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Jumanne Maghembe akionesha hisia ya kushangazwa kuwepo kwa mogogoro kati ya wakulima wadogo wa chai dhidi ya wakulima wakubwa na wenye viwanda ambayo haileti tija ya kuongeza uzalishaji wa chai nchini , wakati alipofungua mkutano wa wadau wa zao hilo mwaka 2011, uliofanyika Julai 8, mwaka huu mjini hapa.
Mmoja wa viongozi wa wakulima wa dogo wa zao la chai nchini , Rehema Malekela ( aliyesimama) akichangia hoja kuhusu hatua za mikakati ya kuboresha zao hilo ili wakulima waweze kupata bei nzuri kwenye masoko ya ndani na nje
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Jumanne Maghembe ( watano waliokaa kulia) akiwa kwenye picha na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Chai Tanzania, Mh. Anne Makinda ( wanne kulia waliokaa) ambaye ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na wadau wengine wa zao hilo, ( wapili kushoto waliokaa ) ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro , Mh. Issa Machibya, sambamba na Wakurugenzi wa Bodi, Wakuu wa Wilaya na Wenyeviti wa Vyama vya wakulima pamoja na Wenye viwanda vya zao la chai nchini.Picha na John Nditi , Morogoro
No comments:
Post a Comment