HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, March 3, 2011

NYUMBANI LOUNGE kufunguliwa rasmi machi 10


Nyumbani Lounge (Gadner G. Habash & Lady Jay Dee) Wanapenda kuwataarifu wateja wao kuwa ufunguzi rasmi wa kiota chao kipya (Nyumbani Lounge) Utafanyika Siku ya Alhamisi ya tar 10 March 2011.

Kutakuwa na kadi za mialiko maalum....... na kwa wengine watakaopenda kushiriki party hiyo ya ufunguzi rasmi kutakuwa na kiingilio mlangoni.

Bei za viingilio zitangazwa Jumatatu Ijayo.

MENU YA BUFFET LA ALHAMIS HII NDANI YA NYUMBANI LOUNGE:

*Supu ya Mboga Mboga
*Muhogo wa Kukaanga
*Wali wa Nyanya
*Kisamvu / Mchicha
*Bamia
*Nyama moto
*Maini na Firigisi
*Red Snapper wa Kukaanga
*Ugali wa Muhogo

Vyakula vyote hivyo kwa pamoja ukipakua katika sahani yako ni 10,000/= (Alfu kumi tu.)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad