HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, March 11, 2011

libeneke la mbeya yetu

salam,

Natumai ya kua utakua mzima wa njema afya mimi pia niko salama kabisa, kwanza hongera sana kwa kazi zako za blog ikiwa ni pamoja na kutuletea habari mbali mbali za nchini kwetu, Duniani burudani na michezo big na Mwenyezi Mungu akubariki uendelee mbele zaidi wewe pamoja na timu yako nzima ya matukio.

Kwa niaba ya timu nzima ya Mbeya yetu blog,tulikua tunaomba msaada wako wa kututambulishia libeneke letu jipya la Mbeya yetu, Tunatanguliza shukrani zetu. Asante sana.

JINA LA BLOG: MBEYA YETU


Tunapenda kulitambulisha wadau wote libeneke jipya la Mbeya Yetu ambapo nia na malengo ni kuwaletea habari mbali mbali kutoka Jijini Mbeya, Tanzania na Duniani kwa Ujumla ikiwa unatukio la aina lolote usisite kututumia kupitia mbeyayetu@yahoo.com . karibuni nyote na asanteni kwa kututembelea.

Kwa pamoja tunaweza.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad