
Waumini wa Dini ya kiislamu wakiandamana leo huku wakiwa wamebebea Bango lenye ujumbe unasomekao
Tunataka Kadhi anayetambulika Kikatiba na si BAKWATA na CCM Kadhi lazima hata kwa Jihad" maandamano hayo yalianzia katika viwanja vya Mnazi Mmoja na kuishia maeneo ya Manzese bahresa jijini Dar es salaam.

Waumini wa Dini ya kiislamu wakifanaya maandamano katika barabara ya Morogoro rodi wakidai mahakama ya Kadhi ikubaliwe.
Wa akina mama wako wapi? Hili swala la mahakama ya kadhi linatakiwa kufanyiwa ufumbuzi wa kutosha, kuna swala la mwizi akikamatwa, talaka, mirathi, elimu, sauti kwa wakina mama na watoto wa kike.
ReplyDeletePia serikali wanaangalia hii mahakama ya kadhi itashirikiana kivipi na vyombo vya dola kuhakikisha haki ya kila mwananchi haivunjwi kwa sababu tu dini inasema kitu fulani.
Na kama ingekua mahakama ya kadhi ndo sababu ya waislam kushindwa kupata maendeleo basi wengine tungeelewa, lakini sio hivyo, sijui kuna sababu gani hasa au faida kubwa ilioje hii mahakama itawasaidia waislamu.
Waislam hebu tuwe na subira kidogo.