
===============================
Rais wa kapuni ya mafuta ya RBP Oil & Industrial Technology Tanzania Limited,Rahma Al Kharoos ametangaza ziara ya timu ya taifa ya wanawake Twiga Stars kwenda nchini Marekani kwa mafunzo mbalimbali wiki ya kwanza ya mwezi Agosti.
Akizungumza kwenye mkutano na wandishi wa habari uliofanyika katika hoteli ya Movenpick jijini Dar es salaam,Rais huyo amesema anaamini kuwa ziara hiyo itakuwa ni chachu ya mafanikio ya timu hiyo wakati itakapokwenda kucheza katika fainali za kombe la mataifa ya afrika kwa wanawake mwezi septemba nchini Afrika Kusini.
Amesema akiwa kama mlezi na mdhamini wa Twiga Stars na kwa kushirikiana na wenyeji wa ziara hiyo huko Marekani ambao ni taasisi ya FREEDOM WASHINGTON wamejipanga kuhakikisha ziara hiyo inakuwa ni ya mafanikio makubwa hasa ukizingatia kwamba timu ya Twiga Stars imeweka historia kwa nchi yetu ya kushiriki kwa mara ya kwanza katika mashindano hayo makubwa ya mpira wa miguu kwa wanawake.
Ameongeza kuwa Twiga Stars ikiwa nchini Marekani itacheza michezo minne na timu za nchi hiyo wa kwanza utakuwa ni wa kuchangia timu hiyo ambapo watu mbalimbali watachangia timu yetu ili iweze kujiandaa vyema na mashindano hayo.
Mama Rahma alisema anaomba wadau, wapenzi wa soka la wanawake kuiunga mkono timu hiyo ya Twiga Stars ambayo imeiletea sifa na heshima ya kubwa taifa letu la TANZANIA kwa kupata nafasi hiyo ya kushiriki michuano mikubwa zaidi barani Afrika kwa wanawake. anasema kwamba anaamini kuwa sasa milango ya wachezaji wanawake kucheza soka la kulipwa nje itatimia.
Rais wa kapuni ya mafuta ya RBP Oil & Industrial Technology Tanzania Limited,Rahma Al Kharoos ametangaza ziara ya timu ya taifa ya wanawake Twiga Stars kwenda nchini Marekani kwa mafunzo mbalimbali wiki ya kwanza ya mwezi Agosti.
Akizungumza kwenye mkutano na wandishi wa habari uliofanyika katika hoteli ya Movenpick jijini Dar es salaam,Rais huyo amesema anaamini kuwa ziara hiyo itakuwa ni chachu ya mafanikio ya timu hiyo wakati itakapokwenda kucheza katika fainali za kombe la mataifa ya afrika kwa wanawake mwezi septemba nchini Afrika Kusini.
Amesema akiwa kama mlezi na mdhamini wa Twiga Stars na kwa kushirikiana na wenyeji wa ziara hiyo huko Marekani ambao ni taasisi ya FREEDOM WASHINGTON wamejipanga kuhakikisha ziara hiyo inakuwa ni ya mafanikio makubwa hasa ukizingatia kwamba timu ya Twiga Stars imeweka historia kwa nchi yetu ya kushiriki kwa mara ya kwanza katika mashindano hayo makubwa ya mpira wa miguu kwa wanawake.
Ameongeza kuwa Twiga Stars ikiwa nchini Marekani itacheza michezo minne na timu za nchi hiyo wa kwanza utakuwa ni wa kuchangia timu hiyo ambapo watu mbalimbali watachangia timu yetu ili iweze kujiandaa vyema na mashindano hayo.
Twiga Stars ilifanikiwa kukata tiketi ya kucheza fainali za kombe la mataifa ya Afrika kwa wanawake itakayofanyika nchini Afrika kusini mwezi septemba mwaka huu baada ya kutoka sale ya magoli 3-3 na timu ya Eritrea.
Mama Rahma alisema anaomba wadau, wapenzi wa soka la wanawake kuiunga mkono timu hiyo ya Twiga Stars ambayo imeiletea sifa na heshima ya kubwa taifa letu la TANZANIA kwa kupata nafasi hiyo ya kushiriki michuano mikubwa zaidi barani Afrika kwa wanawake. anasema kwamba anaamini kuwa sasa milango ya wachezaji wanawake kucheza soka la kulipwa nje itatimia.
No comments:
Post a Comment