
Naibu Mkurugenzi wa Michezo, Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo, Juliana Yesoda (Kushoto) akikabidhi bendera ya taifa kwa nahodha wa timu ya soka ya Taifa ya watoto wa mitaani, Theresia Dominic, kwenye ukumbi wa VIP uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Timu hiyo yenye wachezaji 9 wawili wakiwa ni wasichana, inaondoka nchini leo kuelekea Afrika Kusini kushiriki mashindano ya kombe la Dunia kwa watoto wa mitaani yatakayoanza Machi 14. Kulia ni Rais wa Tanzania Street Children Soccer Academy, Ataf Hirani.picha na Mroki Mroki
No comments:
Post a Comment