.jpg)
.jpg)
Chama cha Japan Karate Association tawi la Tanzania kimeandaa mashindano ya mchezo wa karate kwa vijana wadogo yanayotarajiwa kuanza jumamosi tarehe mosi Novemba mwaka huu katika viwanja vya Don Bosco Youth Centre jijini.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa mikutano wa idara ya habari maelezo mwenyekiti wa chama hicho nchini Daniel Mbega amesema vilabu mbalimbali vitashiriki kwenye mashindano hayo ambayo yataanza kesho jumamosi saa mbili na nusu asubuhi.
Amevitaja vilabu vitakavyoshiriki kuwa ni Scorpion Shotokan karate, Fitness one Karate, Genessis Int. School karate,Chita Karate,Nyuki Karate, Iringa A. Karate na Iringa B. Karate vya mkoani Iringa.
Ameongeza kuwa mashindano hayo yanajumuisha mapambano ya vijana wenye umri wa kuanzia miaka 5 na 6, 7 na 9, 10 na 12, 13 na 15 ambapo zawadi mbalimbali zitatolewa ikiwa ni medali na vikombe, kiingilio kitakuwa shilingi 3.000 na viti maalum itakuwa 5.000 wapenzi wote wa mchezo wa karate manakaribishwa ili kupata burudani.
No comments:
Post a Comment