Na Mwandishi Wetu
WAZIRI Wa Elimu Sayansi Na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda anatarajiwa kuzindua wiki ya elimu,ujuzi na ubunifu inayoendelea katika viwanja vya shule ya sekondari jijini Tanga kesho Agosti 18,2026.
Mkuu wa mkoa huo, Batilda Buriani amesema hayo alipotembelea maonesho hayo na kuongeza kuwa washiriki zaidi ya 300 wapo katika wiki hiyo ambao tayari wamepanga bunifu mbalimbali katika mabanda pamoja na kutoa elimu.
Amewahakikishia wananchi usalama na ulinzi wakati wote wa maonesho na kwamba wanakaribishwa kufika kwa wingi katika viwanja hivyo ili kujifunza kaa kuwa taasisi zote za elimu zikonkatika viwanja hivyo pamoja na taasisi za utafiti.
“Kwa muda wote wa wiki moja kuanzia Agosti 15,2026 hadi Agosti 24,2026 maadhimisho yataanza saa mbili asubuhi na kufugungwa jioni saa 12”, amesema Burian na kuongeza kuwa Waziri Mkuu,Dk Mwigulu Nchemba anatarajiwa kufunga maonesho hayo yenye kauli mbiu elimu,jjuzi,ubunifu njiabya kufikia dira ya Taifa 2050.
Batilda ameongeza kuwa washirikinkatika maonesho hayo ni pamoja na vyuo vikuu,tasisi za tafiti ,vyuo vya elimu na ufundi stad na taasisi binafsi ambazo zinahusiana na sayansi na teknolojia.
Amewataka wananchi kutembelea maonesho hayo kwa kuwa ni nafasi ya pekee kujifunza mambo mbakimbali hara kwa wale wanaotafuta vyuo na usajili.


No comments:
Post a Comment