HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 1, 2025

VIONGOZI, WANANCHI WATAKIWA KUSHIRIKIANA KUDHIBITI MOTO MISITUNI

Na Fredy Mgunda,Mufindi Iringa.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Mufindi, Reuben Chongolo, ametoa wito kwa viongozi na wananchi kushirikiana kwa dhati katika kudhibiti matukio ya moto misituni, akisisitiza kuwa misitu ndiyo uti wa mgongo wa uchumi na ustawi wa jamii.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, Dkt. Linda Salekwa, katika kikao kilichofanyika leo kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Chongolo alisema moto umekuwa ukileta madhara makubwa kwenye mashamba ya miti ya wananchi na yale yanayosimamiwa na Serikali, ikiwemo Shamba la Miti Sao Hill.

“Nchi yetu hasa maeneo yenye misitu tumekua tukipata changamoto kubwa za moto. Lakini kutokana na mikakati ya TFS, tumekuwa na kamati za vijiji zinazoratibu matumizi ya moto, jambo ambalo limeleta manufaa makubwa,” alisema Chongolo.

Aliongeza kuwa ushirikiano kati ya TFS na wananchi ndio silaha pekee ya kuhakikisha misitu inabaki salama na kuendelea kuchangia mapato ya taifa. Pia aliwataka viongozi wa vijiji na kata kuwapa wananchi elimu endelevu kuhusu matumizi salama ya moto hasa kipindi cha kiangazi.

Kwa upande wake, Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill, PCO Tebby Yoramu, alisema TFS imekuwa ikitoa elimu kila mwaka kwa vijiji 60 vinavyozunguka shamba hilo juu ya matumizi sahihi ya moto. Aliwataka wananchi kutoa taarifa za mapema pale wanapoona viashiria vya moto, ili kuepusha madhara makubwa.

Viongozi waliohudhuria kikao hicho waliipongeza TFS kwa jitihada hizo na kuahidi kuendelea kushirikiana katika kutoa elimu na kusimamia uhifadhi wa misitu.

Kikao hicho kilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Mafinga, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, maafisa tarafa, watendaji wa kata na vijiji pamoja na wenyeviti wa vijiji.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Mufindi, Reuben Chongolo, ametoa wito kwa viongozi na wananchi kushirikiana kwa dhati katika kudhibiti matukio ya moto misituni, akisisitiza kuwa misitu ndiyo uti wa mgongo wa uchumi na ustawi wa jamii.
Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill, PCO Tebby Yoramu, amesema kubwa TFS imekuwa ikitoa elimu kila mwaka kwa vijiji 60 vinavyozunguka shamba hilo juu ya matumizi sahihi ya moto na aliwataka wananchi kutoa taarifa za mapema pale wanapoona viashiria vya moto, ili kuepusha madhara makubwa.
Baadhi ya washiriki kikao hicho cha kuzibiti na kupambana na moto katika shamba la miti Zao Hill na maeneo mengine 
Baadhi ya washiriki kikao hicho cha kuzibiti na kupambana na moto katika shamba la miti Zao Hill na maeneo mengine 



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad