
Meneja wa Ofisi ya Kanda ya Kati, Magdalena Mtenga (aliyesimama), akiongea wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Usimamizi wa Maabara za Kemia kwa Wakuu wa Shule za Sekondari wa Jiji la Dodoma (TAHOSSA) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Bustani, Wilaya ya Kondoa, Mkoa wa Dodoma, Septemba 29, 2025.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Sechelela Dodoma, ambaye ni Mwenyekiti wa Wakuu wa Shule za Sekondari (TAHOSSA), Grace Shilly, akimkaribisha Meneja wa Kanda yaKati, Magdalena Mtenga (hayupo pichani) kwa ajili ya kufungua mafunzo ya Usimamizi wa Maabara za Kemia kwa Wakuu wa Shule za Sekondari kutoka Jiji la Dodoma (TAHOSSA) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Bustani Wilaya ya Kondoa,mkoani Dodoma, Septemba 29, 2025.

Mtumishi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Kanda ya Kati, Revocatus Mwamba, akiwasilisha mada juu ya Mfumo wa Ubora ndani ya Maabara za Kemia, Usimamizi na uteketezaji wa Kemikali taka katika mafunzo ya Wakuu wa Shule za Sekondari (TAHOSSA) wa Jiji la Dodoma yaliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Bustani, Wilaya ya Kondoa, Septemba 29, 2025.

Mwakilishi wa Walimu Wakuu wa Kanda ya Kati (TAHOSSA), Peter Mlugu, akiishukuru Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa kutoa Mafunzo ya Usimamizi wa Maabara za Kemia kwa Wakuu wa Shule za Sekondari (TAHOSSA) wa Jiji la Dodoma yaliyofanyika katika Chuo cha Ualimu Bustani, Wilaya ya Kondoa, Septemba 29, 2025.


Baadhi ya Walimu Wakuu walioshiriki mafunzo wakiuliza maswali juu ya majukumu yaMamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali katika mafunzo ya Usimamizi wa Maabara za Kemia kwa Wakuu wa Shule za Sekondari (TAHOSSA) kutoka Jiji la Dodoma yaliyofanyika katika Chuo cha Ualimu Bustani kilichopo Wilaya ya Kondoa, Mkoa wa Dodoma Septemba 29, 2025.


Mkuu wa Shule ya Sekondari Chinyika Wilaya ya Mpwapwa, Nerbert Msyenga, akiomba ufafanuzi juu ya usimamizi wa kemikali taka na uteketetezaji wake katika mafunzo kwa Wakuu wa Shule za Sekondari (TAHOSSA) kutoka Jiji la Dodoma yaliyofanyika katika Chuo cha Ualimu Bustani, Wilaya ya Kondoa, Mkoa wa Dodoma Septemba 29, 2025.


Wakuu wa Shule wakijaza Dodoso la Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikalikuhusu taarifa za Usimamizi wa Maabara za Kemia katika mafunzo kwa Wakuu wa Shule za Sekondari (TAHOSSA) wa Jiji la Dodoma yaliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Bustani, Wilaya ya Kondoa, Dodoma, Septemba 29, 2025.
Wakuu wa Shule za Sekondari (TAHOSSA) wakifuatilia mafunzo ya Usimamizi waMaabara za Kemia yaliyofanyika katika Chuo cha Ualimu Bustani wilayani Kondoa,Mkoa wa Dodoma, Septemba 29, 2025.


Meneja wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Kanda ya Kati, Magdalena Mtenga (watatu kulia, Mstari wa Mbele), akiwa pamoja na viongozi waWakuu wa Shule za Sekondari (TAHOSSA) kutoka wilaya za Dodoma, Chemba, Bahi, Chamwino, Kondoa DC, Kondoa TC, Kongwa na Mpwapwa baada ya mafunzo ya Usimamizi wa Maabara za Kemia katika Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Bustani Wilaya ya Kondoa, Mkoani Dodoma, Septemba 29, 2025.
No comments:
Post a Comment