Mhe.Rwebangira amewasisitiza Watendaji hao kufuatilia mafunzo hayo kwa umakini ili waweze kuelewa kila kinachofundishwa na kutekeleza majukumu yajayo ya Uchaguzi Mkuu wa Ufasaha na weledi.
Mafunzo haya ya siku tatu ambayo yameanza leo tarehe 21 Julai, 2025 yanajumuisha Waratibu wa Uchaguzi wa Mkoa, Wasimamizi wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo, Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi na Maafisa Ununuzi.








No comments:
Post a Comment