HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, July 12, 2025

𝗦𝗨𝗔 𝗻𝗮 𝗟𝗨𝗩𝗔𝗦 𝗸𝘂𝗯𝗮𝗱𝗶𝗹𝗶𝘀𝗵𝗮𝗻𝗮 𝘂𝘇𝗼𝗲𝗳𝘂 𝗸𝗮𝘁𝗶𝗸𝗮 𝘁𝗶𝗯𝗮 𝘆𝗮 𝘄𝗮𝗻𝘆𝗮𝗺𝗮

 



Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo kitaanza kubadilishana wafanyakazi na wanafunzi pamoja na kushirikiana katika tafiti na Chuo Kikuu cha Lala Lajpat Rai cha Tiba ya Wanyama na Sayansi za Afya cha Haryana, India hiyo ni baada ya hafla ya kusaini hati ya makubalinao ya kushirikiana yaliyosainiwa leo Julai 11, 2025 Jijini Dar es Salaam.


Akizungumza baada ya tukio hilo, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo – Utawala Prof. Amandus Muhairwa amesema wamekuwa wakitembeleana na kufanya mazungumzo tangu mwaka 2023 kabla ya kufikia hatua hii ya kusaini makubaliano, yaliyotajwa kuwa chachu katika kuinua uwezo, maarifa na ujuzi wa wataalamu katika kukabiliana na magonjwa ya wanyama ambayo kwa kiasi kikubwa yanafanana baina ya mataifa hayo mawili.

Amesema ushirikiano huo ni juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kudumisha umoja na ushirikiano na taifa la India na kuongeza kuwa teknolojia ambayo imekuwa ikitumika India katika tiba ya wanyama, wataalamu wataongeza maarifa huko na watakuwa kwenye nafasi ya kujifunza na kurejea nchini wakiwa na uwezo mkubwa.





No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad