HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, May 6, 2024

RE/MAX Coastal, Coral Property zazindua mradi wa nyumba za gharama nafuu jijini Dar

 

Waziri wa Ardhi. Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Slaa (wa pili kulia) akikata utepe kuzindua rasmi mradi wa nyumba kwa bei  nafuu wa Sky Royal Jijini Dar es Salaam. Wengine kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Coral Property Holding Co.Ltd  Zhou Tao, Mkurugenzi wa Ardhi wizarani, Upendo Matotola na Mkurugenzi Mkuu wa Hainan International Ltd Li Jun.
James Prevost akizungumza wakati wa kuzindua rasmi mradi wa nyumba kwa bei  nafuu wa Sky Royal Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi  Mtendaji wa Coral Property Holding Zhou Tao akizungumza wakati wa kuzindua rasmi mradi wa nyumba kwa bei  nafuu wa Sky Royal Jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu
KATIKA mpango unaolenga kuunga mkono juhudi serikali za kuhakikisha kunakuwepo na nyumba za makazi bei, kampuni ya ya RE/MAX na ile ya Coral Property zimezindua mradi wa nyumba mpya za bei nafuu wa Sky Royal, mtaa wa Morocco Jijini Dar es Salaam.

Hafla ya uzinduzi wa nyumba hito iliyohudhuriwa na viongozi na wadau mbalimbali katika sekta ya nyumba, ambapo pamoja na mambo mengine, uzinduzi huo ulionyesha dhamira ya dhati ya ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi unaolenga kuwapatia watu makazi ya bei nafuu na yenye ubora wa hali ya juu.

Akizindua mradi huo, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Slaa, ameyapongeza makampuni hayo mawili kwa mpango huo ambao amesema umekuja wakati mufaka haswa ikitiliwa maanani ongezeko la uhitaji wa nyumba za makazi Jijini Dar es Salaam.

"Ujenzi wa nyumba za bei nafuu ni muhimu sana hapa nchini; uamuzi wa kampuni hizi mbili wa kujenga nyumba bora ni mfano bora w akuigwa na taasisi nyingine hapa nchini ili kukabiliana na changamoto inayohusiana na mahitjai ya nyumba bora za makazi”, amesema.

Waziri Silaa aliendelea kusema kuwa, hatua zilizochukuliwa na makampuni hayo mawili zinaunga mkono juhudi za Serikali zinazolenga kuwepo kwa nyumba bora za makazi na za gharama nafuu kwa wananchi hapa nchini.

"Nichukue fursa hii kutoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa hii ya nyumba nzuri za makazi; ni matumaini yangu kuwa uwekezaji wa nyumba nzuri za makazi katika soko kutaiwezesha Serikali kufikia azma yake ya wananchi kuwa na nyumba nchini”, amesema.

Aidha Waziri Silaa ametoa wito kwa makampuni ya RE/MAX Coastal na Coral Property kujiongeza na kupanua panua wigo wa uwekezji wao kwa kuwekeza maeneo mengine hapa nchini ikiwemo Jijini Dodoma ambapo amesema idadi ya watu inakuwa ikongezeka kila siku na hivyo kusababisha ongezeko la mahitaji ya nyumba za makazi na zenye gharama nafuu.

Tukio hilo mbali na kuwa la uzinduzi, pia lilitoa fursa ya washiriki kuona fursa za uwekezaji mzuri na wa uhakika uliofanywa na makampuni hayo.

"Washiriki watapata fursa ya kujionea wenyewe uwekezaji unaohusu nyumba zenye chumba kimoja, viwili na hata vitatu, ambazo zinagharimu kati ya dola za Marekani 81,186, USD 147,427, na USD 191,838; zaidi ya hayo, wawekezaji hao watatoa punguzo la asilimia 8 ya bei ya kila nyumba kama ilivyoorodheshwa, ambapo punguzo hilo litahusu siku ya uzinduzi tu”, imesema taarifa ya pamoja iliyotolewa na uongozi ma makampuni hayo mawili.

Akiongea katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Coral property Holdings Li Jun, amesema, “Uwekezaji huu umelenga kuunga mkono juhudi za Serikali zinazolenga kuhakikisha kunakuwa na nyumba nzuri za makazi na zenye bei nafuu; kupitia miradi ya maendeleo kama vile Sky Royal, pia tunalenga si kuwekeza kwenye nyumba tu, bali pia kuhakikisha wananchi wanakuwa na maisha endelevu, yenye ufanisi na ambayo yatachangia ustawi wa familia kwa ajili ya Watanzania.”

Amesema kampuni yake pia imejikita katika kuhifadhi na kulinda mazingira nakwamba mpango huo ni endelevu. Aidha amesema mradi huo wa Sky Royal unahusu mpango kabambe wa kiteknolojia unaolenga uwekezji wa nyumba bora unaohakikisha mazingira rafiki na kwamba mradi huo umeidhinishwa kituo cha uwekezaji nchini TIC.

Naye, Mkurugenzi wa Kanda wa kampuni ya RE/MAX Pwani, James Prevost, amesema, “Ushirikiano wetu na kampuni ya Coral Property Holdings hususan katika mradi huu wa Sky Royal, umetuwezesha kuwapatia wananchi Jijini Dar es Salaam maisha bora kupitia nyumba nzuri za makazi na zenye unafuu; punguzo la bei siku hii ya uzinduzi pia ni wito kwa wateja kunufaika na uwekezji wa huu mzuri”.

Amesema mradi wa Sky Royal haulengi uwekezaji wa nyumba za makazi tu, bali pia ni kielelezo cha uwekezaji wa nyumba nzuri na za uhakika ambao unalenga kutoa makazi mazuri na endelevu kwa wananchi na kwa bei nafuu.

"Eneo la kimkakati la maendeleo na huduma kamili kwa jamii, inalenga kutengeneza mazingira bora kwa wataalamu wa aina malimbali wakiwemo vijana, kwa wanafamilia na wamiliki wa biashara aina mablimbali," amesema.

Kampuni ya RE/MAX Coastal inasifika kwa utaalamu wake katika maswala ya mauzo na masoko ya majengo, ikiwa na dhamira ya kuwapatia wateja kilicho bora na chenye thamani kulingana na soko lililoko nchini Tanzania.

Kampuni ya Coral Property Holdings imekuwa mstari wa mbele katika kuendeleza uwekezaji wa uhakika wa majengo aina mbalimbali ikiwemo nyumba bora za makazi huku ikizingatia ubunifu wa hali ya juu na endelevu sambamba na ubora wa hali ya juu katika kuhakikisha kunakuweko na suluhisho la uhakika katika sekta ya makazi nchini Tanzania.

Ushirikiano kati ya RE/MAX Coastal na Coral Property Holdings kwenye uzinduzi wa mradi wa Sky Royal ni juhudi za kihistoria zinazolenga kuimarisha mandhari ya jiji la Dar es Salaam.

Kwa kuanisha malengo yao sambamba na ile ajenda ya Taifa inayolenga kuhakikisha uwepp wa makazi bora, kampuni zote mbili zimedhamiria kuimarisha sekta ya ujenzi hususani ujenzi wa majengo aina mbalimbali kwa lengo la kustawisha maisha ya Watanzania wote kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad