HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, December 13, 2023

BASHE:- CHAI YOTE IPITE KATIKA MNADA WA TANZANIA.

Waziri wa Kilimo Mheshimiwa Hussein Bashe (Mb) ametoa maelekezo kwa wakulima wadogo, wakubwa na wanunuzi wote wa chai kuwa chai yote ya Tanzania haitaruhusiwa kuuzwa nje ya utaratibu wa mnada wa Tanzania. Ameyasema hayo leo Desemba 13, 2023 akiwa katika siku ya pili ya ziara yake Mkoani Tanga akizindua kiwanda cha Chai Hai (Organic Tea) cha Sakare kilichopo Bungu wilayani Korogwe.

Mnada wa chai kwa mara ya kwanza ulifanyika Tarehe 13 Novemba, 2023 Jijini Dar es Salaam ambapo kwa kipindi chote huko nyuma Chai ya Tanzania ambayo inasifika kwa upekee wa ubora wa blending imekuwa ikiuzwa katika mnada wa Mombasa jambo ambalo limekuwa mwiba kwa wakulima kwani Chai ya Tanzania katika mnada wa Mombasa imekua haipati bei nzuri na hivyo kuwapunguzia wakulima
mapato.

Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameturuhusu kuanzisha mnada wa chai, ametupatia fedha na kwa kushirikiana wadau wa maendeleo serikali itajenga viwanda vingine Vitano vya kuchakata chai na kukipanua zaidi kiwanda cha Sakare kiweze ku chakata chai nyeusi hasa tukilenga kuwasaidia wakulima wadogo na kuwapa nafasi wakulima wakubwa kupanuka na kuzalisha zaidi katika mashamba yao alisisitiza Bashe, huku akiwapongeza wadau wa maendeleo na watumishi kwa juhudi za kufanikisha mnada huo.

Aidha serikali haitaruhusu uingizwaji wa chai ghafi kutoka nje ya nchi ikiwemo Othordox Tea mbayo kwa miaka yote imekua ikiingizwa nchini kutoka Rwanda. Lengo ni kulinda wakulima wa chai ndani ya nchi kwa kuhakikisha chai yao inapata soko na bei nzuri nchini. Aidha Serikali itaendelea kutatua changamoto mbalimbali za kisoko ili kuimarisha mnada wa chai Dar es salaam alisema Mheshimiwa Bashe.




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad