Mkuu wa Gereza Kihonda, SP. Lucas Mboje akionesha bidhaa za vikapu ambavyo hutengenezwa na wafungwa kwa kutumia mali ghafi zitokanazo na Mkonge katika Gereza Kihonda, Morogoro. Wafungwa hupatiwa ujuzi huo wanapokuwa wakitumikia vifungo katika Gereza hilo.
Mkuu wa Gereza Kihonda, SP. Lucas Mboje akizungumza na wanahabari kuhusiana na shughuli/miradi mbalimbali ya Urekebishaji inayotekelezwa katika gereza hilo walipotembelewa Ofsini kwake, Juni 4, 2023.
Mkuu wa Gereza Kihonda, SP. Lucas Mboje akitolea ufafanuzi Mkonge ulionikwa ikiwa ni mradi ya inayotekelezwa katika Gereza hilo.
Mkuu wa Gereza Kihonda, SP. Lucas Mboje akionesha Mradi wa Fremu za Biashara katika Gereza Kihonda. Fremu hizo ni Moja wapo ya miradi ya ubunifu inayotekelezwa katika Gereza hilo.
Mkuu wa Gereza Kihonda, SP. Lucas Mboje akitolea ufafanuzi kuhusu kituo cha Huduma ya Afya kinachojengwa kwenye
Ujenzi wa Jengo la Waraibu wa Dawa za Kulevya ukiendelea katika hatua za mwisho. Jengo hilo linafadhiliwa na Serikali ya Tanzania, Global Fund kupitia Mamlaka ya Kupambana na Kuthibiti Dawa za Kulevya nchini. Jengo hilo la Kliniki ya Waraibu wa Dawa za Kulevya linajengwa katika eneo la Gereza Kihonda, Morogoro litakuwa na mafunaa makubwa kwani litatoa huduma kwa wafungwa wa mkoa wa Morogoro pamoja na jamii inayozunguka katika Mkoa huo.
Mkuu wa Gereza Kihonda, SP. Lucas Mboje akitlea maelezo Jengo la Waraibu wa Dawa za Kulevya linafadhiliwa na Serikali ya Tanzania, Global Fund kupitia Mamlaka ya Kupambana na Kuthibiti Dawa za Kulevya nchini.
Muonekano wa Kituo cha Afya kinachojegwa katika eneo la Gereza Kihonda, Morogoro litakuwa na mafunaa makubwa kwani litatoa huduma kwa wafungwa wa mkoa wa Morogoro pamoja na jamii inayozunguka katika Mkoa huo.
No comments:
Post a Comment