Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV-Kondoa
KATIBU
Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo amemuelekeza Waziri
wa Maliasili na Utalii kuangalia namna ya kutatua changamoto ya ulipaji
fidia kwa wananchi ambao wameathiriwa na wanyama pori wakiwemo tembo
ambao katika maeneo mengi ya vijiji vinavyozunguka hifadhi wamekuwa
wakilalamika kucheleweshwa kwa fidia pamoja na malipo kidogo.
Chongolo
ameyasema hayo leo Juni 19,2023 alipokuwa akizungumza na wananchi wa
Kata ya Itaswi iliyopo Jimbo la Kondoa Vijijini mkoani Dodoma baada ya
kutembele Shina Namba Sita ambalo liko nyumbani kwa Balozi Msafiri
Antony.
Akiwa
katika kata hiyo Chongolo amepokea malalamiko ya wananchi kuhusu
kuvamiwa na tembo wa hifadhi ya pori la Akiba Mkungunero na hivyo
kuharibiwa mali na mazao yao lakini pia wamekuwa wakicheleweshewa malipo
ya fidia .
Kutokana
na malalamiko hayo , Chongolo amesema ni kweli tembo wamekuwa wengi
kwasababu ya umakini unaofanywa na watu wa uhifadhi lakini suala la
fidia hawajaridhika nalo , hivyo amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kondoa
kuandika orodha ya wananchi wote ambao wameathiriwa na tembo na
atakapoondoka Dodoma awe ameipata orodha hiyo.
“Naomba
nipate orodha hiyo halafu nione huyo mtu anayekwamisha fidia ili
nikapambane naye mbele ya safari.Msiwe na wasiwasi na mtaona matokeo ya
utekelezaji , msiniamini sasa ila mniamini fedha zitakapokuja.Lakini
suala la pili ni ukubwa wa fidia , mtu ana heka 10 mwingine ana heka
mbili wewe roho mbaya ya nini.
“Kwanini
usiandike fidia ya kweli ya mtu wa heka 10 , na mtu wa heka mbili basi
heka mbili, fedha sio zako , athari sio zako wewe uchungu wa kitu
kisicho chako unatoka wapi? Kwanini tunabeba roho mbaya, wewe
unamshahara mwisho wa mwezi lakini unaanza kuhangaika na kumuonea hata
huyu mwenye haki yake ambayo amehangaika kulima anachotaka ni fidia .
“Tuachane
na tabia za ubinafsi na roho mbaya tutengeneze mazingira ya kutenda
haki, mtu mwenye heka 10 apate fidia yake ya heka 10 na mwenye heka 30
apate cha heka 30.Tubadilike na mimi hili jambo nalichukulia kwa uzito
mkubwa, kila unakoenda ambako wananchi wanapakana na hifadhi changamoto
ni kubwa hatuwezi kwenda namna hii,”amesema.
Amesisitiza
atazungumza na wahusika akiwemo Waziri wa Maliasili na Utalii na atampa
orodha ili aishughulikie wananchi wapate fidia wanazostahili huku
akifafanua Waziri hawezi kuchelewa katika kushughulikia changamoto hiyo.
Katibu Mkuu wa CCM Daniel Chiongolo akitoa maelekezo mbele ya Afisa
Muhifadhi na Kamanda wa pori la Akiba Mkungunero Floravick Kalambo
kuhusu malalamiko ya wananchi kuvamiwa na tembo wa
hifadhi ya pori la Akiba Mkungunero,uhalibifu wa mali na mazao
yao ikiwemo na suala la fidia kwa waathirika
Afisa
Muhifadhi na Kamanda wa pori la Akiba Mkungunero Floravick Kalambo
akitoa ufafanuzi wa malalamiko ya wananchi kuhusu kuvamiwa na tembo wa
hifadhi ya pori la Akiba Mkungunero na hivyo kuharibiwa mali na mazao
yao,mbele ya Katibu Mkuu wa CCM pamoja na Wananchi wa Kata ya Itaswi
iliyopo Jimbo la Kondoa Vijijini mkoani Dodoma
Mbunge
wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Waziri wa Uwekezaji, Viwanda
na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji akieleza changamoto mbalimbali
zinazowakera Wananchi mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Daniel Chongolo ili
kuzipatia majibu na ufumbuzi wakati wa kikao cha shina Kata ya Itaswi.Wananchi mbalimbali wakifautilia yaliyokuwa yakijiri kwenye kikao
No comments:
Post a Comment