Benki
ya NMB imeandika historia nyingine baada ya kutwaa Tuzo ya Benki Bora
Tanzania kwa mwaka 2023 wakati wa mkutano wa Africa Bank 4.0 Summit
uliofanyika jijini Nairobi, nchini Kenya kutokana na jitihada ma
utendaji kazi wa benki hiyo katika kuimarisha uchumi wa Tanzania kwa
kutoa suluhu za kidijitali na huduma bora.
Tuzo
hiyo ilizingatia nyanja zote za utoaji wa bidhaa na huduma za benki
ambazo zinazojumuisha utoaji wa huduma kwa wateja wa rejareja pamoja na
utoaji wa huduma za kidijitali.
Katika
hafla hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki hiyo Ruth Zaipuna pia
alinyakua Tuzo ya Mkurugenzi Mtendaji Mkuu (CEO) Bora wa Tanzania 2023
kwa mwaka wa pili mfululizo baada ya kuibuka mshindi wa tuzo hiyo ya
kifahari wakati wa mkutano wa mwaka jana.
Tuzo
za Africa Bank 4.0 hutambua juhudi na uvumbuzi wa wadau vinara barani
Afrika katika sekta za kibenki, huduma za kifedha pamoja na sekta ya
bima.
Akizungumza
mara baada ya kupokea tuzo hizo kwa niaba ya benki hiyo, Afisa Mkuu
Rasilimali Watu wa Benki ya NMB, Emmanuel Akonaay alisema Tuzo hiyo ya
Benki Bora Tanzania 2023 ni ushahidi tosha wa dhamira ya benki hiyo
katika kuendeleza ubunifu na kukidhi mahitaji ya wateja wake huku
akihidhinisha kuwa inaendana na utamaduni wa ubora wa benki hiyo
unaolenga kutoa huduma za kibunifu na kipekee kwa wateja wake sambamba
na matumizi ya teknolojia ya kisasa.
“Nina
furaha kubwa kupokea tuzo hii kwa niaba ya benki. Kushinda tuzo hii
inathibitisha kwamba tumeanza kufikia ndoto yetu ya kutoa huduma zenye
viwango vya juu ambazo tumekuwa tukizitoa kwa maika nyingi . Natoa tuzo
hii kwa wafanyakazi wenzangu wa benki ya NMB kwa jitihada zao na
kujitolea kwao kwani jitihada zao zimeleta heshima hii kwa benki yetu.
Tunaelewa umuhimu wa kutoa huduma za kipekee kwa wateja wetu hivyo
tumekuwa tukibuni huduma mpya kila mara ilikuboresha na kuridhisha
wateja wetu,” Akonaay alisema.
Akoonay
alisema benki hiyo kwa miaka mingi imefanikiwa kuwa mstari wa mbele wa
kutoa huduma bora kwa wateja wake, huku ikianzisha dhana za kibunifu
ambazo pia zimesaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha utendaji kazi wake.
“Kama
kinara katika sekta ya kibenki hapa nchini Tanzania, tunajivunia kuwapa
wateja wetu huduma za kibenki ambazo zinaendana na viwango vya
kimataifa. Benki yetu ya NMB inaendelea kutengeneza fursa za kifedha kwa
kila mtu na hu ndio msingi wa dhamira yetu. Tutaendela kuongeza nguvu
zaidi ya watu wetu na rasilimali zetu ili kufanya kazi na kuongeza
ushirikishwaji wa kifedha, "aliongeza.
Tuzo
hizo mbili zimepatikana miezi michache baada ya benki hiyo kutangaza
faida ya kihistoria baada ya makato kodi iliongezeka kwa asilimia 47
hadi shilingi bilioni 429 ukilinganishwa na bilioni 290 iliyopatikana
mwaka 2021 na kuifanya banki ya NMB kushika nafasi ya 3 bora katika
Ukanda wa Afrika Mashariki kwa faida.
Wakati
huo huo, mali za benki hiyo zilifikia kilele cha zaidi ya shilingi 10
kutoka trilioni 5.5 miaka minne iliyopita huko msingi wa amana ukipanuka
hadi trilioni 7.5 kutoka trilioni 4.2 trilioni katika miaka mitatu tu.
Matokeo
mazuri ya kifedha ya mwaka 2022 yanaonyesha kasi kubwa ya utendaji kazi
ambayo NMB imekuwa nayo katika miaka minne iliyopita na ubora katika
utoaji wake wa huduma za Kibenki.
Akizungumzia
tuzo ya Mkurugenzi Mtendaji Bora, katika taarifa fupi iliyotolewa na
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Ruth Zaipuna jijini Dar es Salaam
alisema, “Kwa unyenyekevu mkubwa, nakushukuru sana kuwa mpokeaji wa Tuzo
ya Mkurugenzi Mtendaji Bora wa mwaka 2023 nchini Tanzania ambayo
inatambua mafanikio na mchango wangu kama kiongozi. Najivunia kuendelea
kuongoza taasisi yenye sifa kubwa ambayo inaendelea kujiweka katika
nafasi kuendelea kuweka na alama ya kimataifa kwa ubora,”
Zaipuna
alitoa tuzo hiyo kwa wafanyakazi wenzake wa Benki ya NMB, menejimenti,
bodi ya wakurugenzi, wateja na wadau waoshirikiana na benki yake.
“Natumia
muda huu kuwashukuru wadau wetu wote kwa kuendelea kushirikiana nasi na
juhudi zao zimetuwezesha kuendelea kuhudumia jamii,” aliongeza.
Afisa Mkuu Rasilimali Watu wa Benki ya NMB, Emmanuel Akonaay (kushoto), akimpongezwa na Mkurugenzi
wa Kampuni ya BII World, Fahd Ali Akmal (kulia) baada ya NMB kushinda
tuzo ya Benki Bora Tanzania 2023 pamoja na tuzo ya CEO Bora Tanzania
iliyokwenda kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna.Hafla
hiyo ilifanyika hoteli ya Radisson Blue iliyopo jijini Nairobi, Kenya
mwishoni wa wiki iliyopita.
Afisa
Mkuu Rasilimali Watu wa Benki ya NMB, Emmanuel Akonaay (kulia),
akipokea tuzo ya CEO Bora Tanzania 2023 kutoka kwa Mkuu wa Idara ya
Mauzo Kampuni ya Tribe, Katrina Harding kwa niaba Mkurugenzi Mtendaji wa
Benki ya NMB, Ruth Zaipuna. NMB pia imeibuka mshindi wa Tuzo ya Benki
Bora Tanzania 2023. Hafla hiyo ilifanyika hoteli ya Radisson Blue
iliyopo jijini Nairobi, Kenya mwishoni wa wiki iliyopita. Kushoto ni
Mkurugenzi Mtendaji na Mwanzilishi wa Fintech Tribe Mo Harvey.
No comments:
Post a Comment