Na Mwandishi Wetu
WANACHAMA
zaidi ya 250 wa Chama Cha Wamiliki wa Malori Tanzania (TATOA)
wanatarajia kushiriki kwenye mkutano Mkuu wa Chama hicho utakaofanyika
hapo kesho Jumamosi jijini Dar es Salaam, ambapo Waziri wa Ujenzi na
Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa atakuwa mgeni rasmi.
Akizungumza
na Waandishi wa habari jijini Dar es Salaamu,Mwenyekiti wa TATOA
amesema kuwa mkutano wao wa Saba wa mwaka utafanyika katika Hoteli ya
Johari Rotana na madhumuni ya mkutano huo ni kuwaleta wasafirishaji wote
wa sekta ya uchukuzi pamoja ili kujadili masuala mbalimbali
yanayohusiana na sekta ya usafirshaji.
"Hii inajumuisha changamoto zote zinazoikabili
sekta
ya usafirishaji. Mkutano huo utajumuisha wadhamini ambao watakuwa
wakiwasilisha,kuonesha bidhaa na huduma zao ambazo zinaongeza utendaji
kazi katika sekta ya usafirishaji..
"Wadhamini
hao kwa pamoja ni Total Energies, benki ya NBC, Double Click, UTrack,
GF trucks & equipment na korridor. TATOA ni chama cha hiari cha
wafanya biashara yakusafirisha mizigo kwa njia ya barabara ndani na nje
ya Tanzania, hususani katika nchi zilizo katika kanda ya jumuiya ya
kusini wa Afrika (SADC).
"Na
jumuiya ya AfrikaMashariki (EAC).DRC (Katanga, Mikoa ya Kivu ya
Kaskazini na Kusini), Zambia, Malawi,Zimbabwe, Rwanda, Burundi, Uganda,
naSudan Kusini. Ilianzishwa mwaka 2005 ikiwa na wanachama 25 pekee.TATOA
imekua na kuwa chama cha wafanyabiashara waliojitolea ambao wanaona
sekta ndogo ya usafirishaji wa barabara inakuwa mchangiaji namba 2 wa
Pato la Taifa kuwa na wanachama zaidi ya 900," alisema Lukumay .
Aidha
Lukumay alifafanua kuwa Mkutano Mkuu wa 7 wa Mwaka wa TATOA unatarajia
kuhudhuriwa zaidi ya Wanachama 250 ambao ni wamiliki wa kampuniza
usafirishaji . Wafadhili kutoka Totalengies, Benki ya NBC,
Doubleclick-U-track, GFtrucks and equipment, korridor watatoa suluhisho
ya mambo mbali mbali yanayohusiana na sekta , hiyo ni kupitia maonesho
ya bidhaa pamoja na huduma wanazotoa.
Kwa
upande wake Meneja Masoko na Mawasiliano wa GF Trucks and Equipment,
Smart Deus, aliwahimiza wanachama wa chama hicho kujitokeza kwa wingi
katika mkutano huo huku akieleza kuwa wana ofa mbalimbali kwa ajili ya
wateja wao.
"Katika
mkutano huo tutatangaza kampeni maalum ya kutoa huduma za kiufundi bila
malipo kwa malori yanayopita katika Barabara kuu ya Morogoro kwenda
nchi jirani," Alisema Deus.
Katika
hatua nyingine Meneja wa kitengo cha vilainishi kutoka Total Energies,
Ally Saleh amesema kampuni hiyo imekuwa ikifanya kazi kwa karibu na
TATO.
"Kwetu
sisi wasafirishaji ni wengi kuliko wateja kwa sababu licha ya kununua
mafuta na mafuta kutoka kwetu tunawafuatilia ili kuhakikisha vifaa vyao
vinafanya kazi ipasavyo na kwa ufanisi," alisema Salehe
Mgeni
rasmi katika mkutano huo atakuwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof
Makame Mbarawa na wakuu wa mashirika mbalimbali ya serikali ikiwemo,TPA,
TRA, LATRA, EWURA, TANROADS, GCLA, TASAC. Wanachama pia watapata fursa
ya kuunganishwana wanachama wengine kutoka katika sekta hiyo
ya usafirishaji.
Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Malori Tanzania (TATOA), Elias Lukumay akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mkutano mkuu wa mwaka kujadili changamoto zao mbalimbali utakaofanyika jijini Dar es Salaama kesho Jumamosi.
Mwenyekiti
wa Chama cha Wamiliki wa Malori Tanzania (TATOA), Elias Lukumay
akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mkutano mkuu wa
mwaka kujadili changamoto utakaofanyika jijini Dar es Salaama
kesho.Kulia ni Meneja masoko na mawasiliano wa kampuni ya GF Trucks
& Equipments Ltd Smart Deusi na katikati ni Mkurugenzi mwendeshaji
wa kampuni ya Double luck consulting ltd, Sandeep Basra na kushoto ni
Meneja wa kampuni ya Total Energies, Ally Saleh
Meneja
Masoko na Mawasiliano wa kampuni ya GF Trucks & Equipment’s Ltd,
Smart Deusi akizungumza na wandishi wa habari kuhusu maandalizi ya
mkutano mkuu wa Chama cha Wamiliki wa Malori Tanzania (TATOA) kujadili
changamoto mbalimbali utakaofanyika jijini Dar es sdalaam kesho, Kushoto
ni Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Malori Tanzania (TATOA), Elias
Lukumay na katikati ni Mkurugenzi mwendeshaji wa kampuni ya Double luck
consulting ltd, Sandeep Basra.
Meneja
wa kampuni ya Total Energies, Ally Saleh akizungumza na wandishi wa
habari kuhusu maandalizi ya mkutano mkuu wa Chama cha Wamiliki wa Malori
Tanzania (TATOA) kujadili changamoto mbali mbali utakaofanyika jijini
Dar es sdalaam kesho.Wengine ni Mwenyekiti wa Chama hicho, Elias Lukumay
, Mkurugenzi mwendeshaji wa kampuni ya Double luck consulting ltd,
Sandeep Basra na kulia ni Meneja masoko na mawasiliano wa kampuni ya GF
Trucks & Equipment’s Ltd Smart Deusi .
Friday, January 20, 2023

Home
HABARI
WAZIRI MBARAWA KUSHUHUDIA WADAU WA SEKTA YA USAFIRISHAJI WAKIKAA MEZA MOJA KUTATUA CHANGAMOTO ZAO KESHO JIJINI DAR
WAZIRI MBARAWA KUSHUHUDIA WADAU WA SEKTA YA USAFIRISHAJI WAKIKAA MEZA MOJA KUTATUA CHANGAMOTO ZAO KESHO JIJINI DAR
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment