HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, January 14, 2023

 CMSA YATOA NENO UORODHESHWAJI HATIFUNGANI YA BENKI YA KCB

 MAMLAKA ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) amesema  uorodheshwaji wa hatifungani ya Benki ya KCB yaani KCB Fursa Sukuk, ni miongoni mwa sehemu ya maendeleo katika sekta ya fedha hapa nchini na inaweka historia ya kuwa hatifungani ya kwanza inayokidhi misingi ya Shariah kutolewa kwa umma na kuorodheshwa katika Soko la Hisa la Dar es Salaam, na ambayo imeidhinishwa na Mamlaka hiyo.


Akizungumza Januari 13,2023 jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kuorodheshwa kwa hatifungani inayokidhi misingi ya shariah kwenye soko la hisa la Dar es Salaam ,Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka hiyo, CPA Nicodemus Mkama amesema Oktoba 25, 2022 CMSA ilidhinisha Benki ya KCB kuuza hatifungani inayokidhi misingi ya shariah.

"Yaani KCB Fursa Sukuk, yenye thamani ya Sh. bilioni 10 na ongezeko la Sh.bilioni 5.Idhini ilitolewa na CMSA baada ya Benki ya KCB kukidhi matakwa ya Sheria ya Masoko ya Mitaji na Dhamana Sura ya 79 ya Sheria za Tanzania. Pia na Miongozo ya Masoko ya Mitaji na Dhamana ya Utoaji wa Hatifungani ya mwaka 2019 ambapo pamoja na mambo mengine, KCB ilitakiwa kuwa, Waraka wa Matarajio wa utoaji wa hatifungani ya Fursa Sukuk.

"Kuidhinishwa na Bodi ya Ushauri wa Shariah (Shariah Advisory Board) ya benki ya KCB na kupata ithibati kutoka kwa kampuni yenye utaalam kuhusu uwekezaji unaokidhi Misingi ya Shariah.Benki ya KCB ilikidhi matakwa haya kwa kuwa na Bodi ya Ushauri wa Shariah ambayo ni KCB Sahl Shariah Advsory Board na ithibati ilitolewa na Kituo cha ushauri kuhusu uwekezaji unaokidhi Misingi ya Shariah."

Amesema Mauzo ya hatifungani ya Fursa Sukuk yalifunguliwa Novemba 9, 2022 na kufungwa  Desemba 5 , 2022, ambapo kiasi.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA),CPA Nicodemus Mkama 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad