Msimu wa nne wa kampeni ya
NMB MastaBata tayari umeanza baada ya promosheni hiyo ya kuchagiza
malipo kidijitali kuzinduliwa Mbeya Ijumaa huku sehemu ya zawadizenye
thamani ya TZS milioni 350 ikipangwa kutumika kuwawezesha wateja
kiuchumi.
Kiasi cha
TZS milioni 173 na pikipiki 14 zitatumika kuwakwamua kiuchumi washindi
wa shindano hilo linalojulikana mara hii kama NMB MastaBata, Kote-Kote!
Kwa mujibu wa Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Bw
Filbert Mponzi,utaratibu huo utasaidia kuimarisha vipato vya wateja
watakaoibuka washindi.
MastaBata
ya mwaka huu itaua ndege wawili kwa jiwe moja. Itahamasisha matumizi
zaidi ya kadi za NMB Mastercard na Lipa Mkononi(QR) na kuwapa fursa
wateja kuboresha uchumi wao.
“Tofauti
na mwaka jana, mwaka huu tumeamua kuwa na zawadi ya fedha pamoja na
pikipiki sababu tunahitaji sio tu kuhamasisha matumizi ya kadi lakini
pia kuwa chachu ya mabadiliko ya kiuchumi ya wateja wetu, tunaamini
pikipiki hizi zinakwenda kutumikakatika biashara na kuongeza kipato cha
washindi wetu,” Bw Mponzi alibainisha.
Zawadi
kubwa itakayohitimisha kampeni ya NMB MastaBata, Kote-Kote ni washindi
saba kujishindia tiketi za kusafiri kuelekea Dubai pamoja na wenzi wao
kwa siku nne Kupitia zawadi hizo, NMB inataka na msimu unaokuja wa
Krismasi na Mwaka Mpya kufana zaidi kwa wateja wake, na kusema kwani
kila wiki wateja 75 watajishindia TZS 100,000 kila mmoja, Pikipiki moja
na kila mwezi 1,000,000 kila mmoja na Pikipiki 2 hivyo jumla Pikipiki
14.
Mgeni rasmi wa
uzinduzi huo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dr Rashid
Chuachua,aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa, Bw Juma Homera na kuipongeza NMB
kwa kuwa mshirika wa dhati wa maendeleo kuchangia ustawi wa jamii.
Huu
ni mwaka wa wanne mfululizo wa kampeni za NMB kwa kushirikiana na
kampuni ya Mastercard kuhamasisha malipo bila kutumia pesa taslimu.
Mchakato huu ulianza na MastaBata mwaka 2018, kisha MastaBata Siyo
Kikawaida na kampeni ya mwaka janailikuwa ni MastaBata – KivyakoVyako.Mkuu
wa wilaya ya Mbeya Dr. Rashid Chuachua (wapili kulia) akifurahia baada
ya kuzindua rasmi kampeni ya NMB Mastabta – Kotekote iliyozinduliwa
kitaifa mkoani Mbeya yenye lengo la kuhamasisha malipo ya bidhaa na
huduma kwa kutumia kadi, kuskani QR (Lipa Mkononi) na malipo ya
kimtandao. Benki ya NMB Imetenga zawadi za zaidi ya milioni 300 kwaajili
ya kampeni hii. Wapili kushoto ni Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na
Biashara wa benki ya NMB, Filbert Mponzi, kulia ni Afisa Mkuu wa
Rasilimali watu wa benki hiyo, Emmanuel Akonaay na kushoto ni Mkuu wa
Idara ya Kadi, Philbert Casmir.
No comments:
Post a Comment