HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, October 18, 2022

MALKIA MAXIMA AWASILI DAR ES SALAAM KWA ZIARA YA KIKAZI

 


Malkia wa Uholanzi, Malkia Maxima amewasili Jijini Dar es Salaam akitokea mkoani Kilimanjaro ambapo alianzia ziara yake jana tarehe 17 Oktoba 2022 baada ya kuwasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 17 – 19 Oktoba, 2022.

Mara baada ya Malkia Maxima kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam, alipokelewa na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Robert Kahendaguza.

Malkia Maxima ambaye pia ni Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Mfumo Jumuishi wa Fedha katika Maendeleo anatarajia kukutana kwa mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan tarehe 19 Oktoba 2022.

Mbali na kukutana na Mhe. Rais Samia pia Malkia Maxima kabla ya kuhitimisha ziara yake hapa nchini, anatarajia pia kukutana na viongozi mbalimbali waandamizi wa Serikali.

Malkia wa Uholanzi, Malkia Maxima akipokelewa na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Robert Kahendaguza baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam
Malkia wa Uholanzi, Malkia Maxima akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam. Pembeni yake mwenye suti ya kijivu ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Robert Kahendaguza
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Robert Kahendaguza akiteta jambo na Malkia wa Uholanzi, Malkia Maxima baada ya Malkia kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam
Malkia wa Uholanzi, Malkia Maxima akimueleza jambo Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Robert Kahendaguza baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad