HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, October 28, 2022

BIDHAA NYINGI NA ZENYE UBORA KUTOKA TANZANIA ZAANZA KUPATA SOKO NCHI ZA ULAYA

 Na Mwandishi Wetu, Ufaransa

KUTOKANA  na juhudi zinazofanywa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, bidhaa nyingi na zenye ubora kutoka Tanzania zimeanza kupata masoko katika nchi za Ulaya. 

Hayo ni maparachichi kutoka Tanzania ambayo yanauzwa katika "supermarket" kubwa iitwayo Carrefour mjini Paris, Ufaransa. Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ufaransa unatoa mwito kwa wakulima na wafanyabiashara nchini Tanzania waandelee kuzalisha  kwa wingi bidhaa zenye ubora kwa ajili ya masoko ya nchi za Ufaransa, Uhispania na Ureno.

Kwa mujibu wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ufaransa umeeleza kwamba "Tunawaomba wakulima na wafanyabiashara wa aina mbalimbali kuzalisha kwa wingi bidha nyingi na zenye ubora, soko katika nchi za Ulaya ni kubwa, hivyo ni wakati wetu kutumia soko hilo kuuza bidhaa za kutoka nyumbani."ni 


 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad