HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, September 13, 2022

MAKAMU WA RAIS AZINDUA JENGO LA SARATANI BUGANDO MWANZA

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akizindua Jengo la Wodi ya Wagonjwa wa Saratani katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando Jijini Mwanza leo tarehe 13 Septemba 2022. Kushoto ni mke wa Makamu wa Rais Mama Mbonimpaye Mpango na Askofu wa Jimbo la Kigoma Mhashamu Joseph Mlola, Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Bugando Dkt. Fabian Massaga na Kulia ni Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel na Askofu wa Jimbo la Mwanza Mhashamu Renatus Nkwande.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akizungumza na wananchi mbalimbali waliofika kupata tiba katika Jengo la Wodi ya Wagonjwa wa Saratani katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando Jijini Mwanza mara baada ya uzinduzi wa Jengo hilo leo tarehe 13 Septemba 2022.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akiagana na Askofu wa Jimbo la Kigoma Mhashamu Joseph Mlola wakati alipomaliza shughuli ya Uzinduzi Jengo la Wodi ya Wagonjwa wa Saratani katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando Jijini Mwanza leo tarehe 13 Septemba 2022. Kulia ni Askofu wa Jimbo la Mwanza Mhashamu Renatus Nkwande.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad