Na Mwandishi wetu,Dar es Salaam.
Kampuni
ya Bima ya Phoenix Assurance imezindua huduma ya BimaPlus kwa wamiliki
wa magari makubwa ya usafirishaji wa bidhaa mbalimbali ndani na nje ya
nchi.
BimaPlus itawawezesha wafanya biashara hao kulipwa fidia ya
bidhaa zao na gari husika endapo watapatwa na majanga mbalimbali
(ajali) wakiwa njiani.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Phoenix
Assurance Bw Ashraf Musbally alisema kuwa lengo kubwa la huduma hiyo ni
kulinda mtaji wa mfanyabiashara kwa wateja wao watakao jiunga na bima
kubwa au Comprehensive.
Bw. Musbally alisema kuwa wafanyabiashara
wa bidhaa mbalimbali zinazokwenda mikoani au nje ya nchi wanakuwa na
wakati mgumu wa mali zao kufika salama kutokana na matatizo mbalimbali
ikiwa pamoja na wizi.
Alisema kuwa kupitia BimaPlus, mfanya biashara atakuwa na uhakika wa mali zake ikiwa pamoja na chombo cha usafirishaji.
“Kupitia
BimaPlus, msafirishaji atakuwa na uhakika wa mali na mtaji wake kwani
kampuni yetu itakuwa tayari kulipa fidia endapo kutatokea mali husika
kupotea,” alisema Bw Musbally.
Alisema kuwa huduma hiyo ni muhimu
kwa wafanyabiashara na kuwaomba kujiunga nayo kwani inalpa fidia kwa
dereva, utingo, mmliki wa mzigo na mjanga ikiwa mke au mume wa mnufaika
ambao watafidiwa kiasi cha sh mlioni 2.
“Uanzishwaji wa huduma
ya BimaPlus ni muendelezo wa ubunifu na upanuaji wa shughuli zetu katika
soko la bima hapa nchini. Lengo letu ni kumfaidisha mteja wetu na kuwa
na amani katika shughuli zake. Kupitia kwa BimaPlus, mteja wetu atakuwa
na uhakika wa biashara yake kwa sababu mali (bidhaa) zitakuwa salama na
vilevile chombo cha usafirishaji. Kampuni yetu italipa fidia kwa
majanga yoyote yatakayotokea,”alisema Bw.Musbally alisema kuwa huduma ya
BimaPlus pia inamlipa fidia dereva na wafanyakazi wengine katika gari
husika ebdapo watakuwa wamepata ajali.
Alisema kuwa pia BimaPlus
inalipa fidia nyingi endapo muhusika atapata wakati wa usafirishaji wa
bidhaa husika na vile vile italipa fidia ya gharama za usalama au
ulinzi. Alisema kuwa kampuni yao imejipanga kuendeleza huduma ya bima
nchini na ndiyo maana wamekuwa wabunifu kwa lengo la kumnufaisha mteja.
“Phoenix
imekuwa mwanzilishi wa ubunifu wa bidhaa zilizopo kwani ilikuwa ya
kwanza kuja na ubunifu kama vile huduma ya Usaidizi wa Barabara ambayo
ni utulivu.
Alisema ili kutoa huduma za haraka, wameanzisha
kitengo cha huduma ambacho kinafanyakazi masaa 24 na watakuwa wanalipa
fidia kwa muda usiozidi siku 30.
Kwa upande wake, Meneja wa Kanda
ya Mashariki wa Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima Nchini (TIRA),
Bw Frank Fred aliipongeza kampuni ya Phoenix Assurance kwa kuanzisha
bima hiyo ambayo inaleta suluhisho kwa wafanyabiashara wasafirishaji
nchini.
Bw Fred alisema kuwa bima hiyo inawapa uhakika wafanyabiashara wa sekta ambayo imekuwa na changamoto kadhaa.
Alisema
kuwa bima hii ya BimaPlus itachangia katika kujenga uchumi nchini na
TIRA itaendelea kuunga mkono jitahada na ubunifu wa Phoenix Assurance
katika kuleta maendeleo nchini.
Wakati huo huo; Kamanda Msaidizi
wa Usalama barabarani hapa nchnim Kamishna msadizi wa Polisi ACP Meloe
Buzema alisema kuwa bima hiyo inaleta chachu ya maendeleo ya sekta hyo
hapa nchini.
“Nawapongeza kampuni ya Phoenix kwa kuanzisha bima
hiyoambayo inaleta faraja kwa wafanyabiashara wa usafirishaji na
kuwajali madereva pia,” alisema ACP Buzema.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa kampuni ya bima ya Phoenix Assurance Bw. Ashraf
Musbally (kushoto) akizungumza wakati wa uzinduzi wa bidhaa mpya ya
BimaPlus yenye lengo kubwa la kulinda mtaji wa wafanyabiashara wa
usafirishaji mizigo.
Meneja
wa Kanda ya Mashariki wa Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima
Nchini (TIRA), Bw Frank Fred akizungumza wakati wa uzinduzi wa bidhaa
mpya ya BimaPlus yenye lengo kubwa la kulinda mtaji wa wafanyabiashara
wa usafirishaji mizigo.
Kamanda
Msaidizi wa Usalama barabarani hapa nchini Kamishna msadizi wa Polisi
ACP Meloe Buzema akizungumza wakati wa uzinduzi wa bidhaa mpya ya
BimaPlus yenye lengo kubwa la kulinda mtaji wa wafanyabiashara wa
usafirishaji mizigo.
Meneja
Mkuu wa kampuni ya bima ya Phoenix Assurance Bw. Robert Kalegeya
akizungumza wakati wa uzinduzi wa bidhaa mpya ya BimaPlus yenye lengo
kubwa la kulinda mtaji wa wafanyabiashara wa usafirishaji mizigo.
No comments:
Post a Comment