Na mwandish wetu
Dar
es Salaam. Kampuni ya kuunganisha magari nchini, GFA leo imeunganisha
gari la 600 ikiwa ni miaka miwili tangu ianze shughuli hiyo Septemba
mwaka 2020.
Akizungumza katika sherehe za kuadhimisha miaka 15 ya
kampuni hiyo, Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Dk Ashatu
Kijaji, amesema kiwanda hicho kimeifaya Tanzania kutimiza moja ya
itifaki za kuwa katika eneo huru la biashara Afrika.
"Tulikuwa
wapokeaji lakini hatukuwa na kiwanda cha kuunganisha magari, GF Truck
imetufanya tuwe na cha kusema tunapoingia katika vikao vya kiitifaki vya
eneo huru la biashara la Afrika," amesema.
Kwa upande wake,
Mkurugenzi Mtendaji wa GF Trucks, Imran Karmari alisema kampuni hiyo
ilianza kuunganisha gari la Kwanza Septemba 2020 na hadi sasa
imeshaunganisha magari 600.
"Mara ya kulikuwa na mashaka kwamba Watanzania tutaweza na bidhaa zitakuwa na ubora, lakini hadi hatua hii tumeweza," amesema.
Kampuni ya GF Trucks & Equipment’s Ltd ilianza mwaka 2007 ikiwa na wafanyakazi wanne na haikuwa na ofisi.
Alisema
kwa sasa asilimia 80 ya malighafi za kuunganisha magari wanaagiza
kutoka China huku asilimia 20 pekee ndiyo zinazotoka ndani.
"Bado
Tanzania hakuna Viwanda vya malighafi ya kuunganisha magari ndiyo maana
tunaagiza, lakini mipango yetu ya baadaye ni sisi wenyewe kuanzisha
kiwanda," alisema.
Hata hivyo, alisema jumla ya watu 300 wameajiriwa moja kwa moja katika kampuni hiyo yenye makao makuu yake Kibaha mkoani Pwani.
Tunajivunia
kuwa Kampuni ya kwanza nchini kuwa na kiwanda cha kunganisha magari
na wakati tunaanza hatukutegemea kama tutafika siku kama leo kutikiza
idadi ya magari 600.
Pia lengo la kampuni ni kuweza kuunganisha
magari ya aina zoote ingawa kwa sasa tunaunganisha Truck pekee na
tunashukuru FAW na HONG YANG kwa kutuamini na kuweza kunganisha magari
katika kiwanda chetu.
No comments:
Post a Comment