Mwinjilisti wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Usharika wa Boko, Marry Kombe (kulia), akimkabidhi Mkurugenzi Huduma za Uuguzi na Ukunga wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Zuhura Mawona, sehemu ya zawadi zilizotolewa na Wanawake wa KKKT Usharika wa Boko. Vitu vilivyokabidhiwa ni jokofu moja, mashuka 100, viyoyozi (AC) viwili, pamoja na kifaa cha kuzuia moto katika jokofu vikiwa na thamani ya shilingi milioni 4.4.
UMOJA wa Wanawake wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Boko Jijini Dar es Salaam leo Juni 25, 2022 wamewatembelea na kuwafariji watoto wanasumbuliwa na maradhi ya saratani waliolazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kitengo cha watoto wanaougua saratani.
Mkurugenzi Huduma za Uuguzi na Ukunga wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Zuhura Mawona (kushoto), akizungumza wakati wa kupokea zawadi zilizotolewa na Wanawake wa KKKT Usharika wa Boko kwa ajili ya watoto wanaoendelea na matibabu ya saratani katika hospitali hiyo. Vitu vilivyokabidhiwa ni jokofu moja, mashuka 100, viyoyozi (AC) viwili, pamoja na kifaa cha kuzuia moto katika jokofu.![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjU6uAowWMIHaNhUyyLzNzW9tAZne-tsX7sXHQbegVcqPEHm52hTooiLzruJMXPSD6O_lscxEeEE-uF9YjsEZkl22jn3q1_KF4HfN2QCH6DO99RTRZWbGVoxPrnDMyhIctjIjwS5IHcVVO6j5jgOKI8keeyS-_Dvi-THGNbZSqjK88t6muWjFDOxxwiiA/w640-h426/_P5A3593.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjU6uAowWMIHaNhUyyLzNzW9tAZne-tsX7sXHQbegVcqPEHm52hTooiLzruJMXPSD6O_lscxEeEE-uF9YjsEZkl22jn3q1_KF4HfN2QCH6DO99RTRZWbGVoxPrnDMyhIctjIjwS5IHcVVO6j5jgOKI8keeyS-_Dvi-THGNbZSqjK88t6muWjFDOxxwiiA/w640-h426/_P5A3593.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj7W7UNMUxyxT6_1K8souDesWP-d7VA5mJ2yENGVihw2ffResCiFWB1xykmQB35uTkalJgqxf517xquEvXKUyS5c-yXFAf2peKn1TwubEVwl0kmpK9g7yBIvMjjWhsKt96z2pcKjgVvjoITVec74fj75O0UEwD5pHXUAL4xNKlf1LnsYvKeZUOUsmnu1g/w640-h426/_P5A3601.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi39f2qBw2jIz3UxDhjo5K3m9Gamt91HD-VP36qH0zDHe95qadz582EGCB0wTN4N2fUsVxCTebwAw4ZfxVQ5_LHMj8Bz--aVb3W8d2yq6JwiSlMAoXfJBG1VUTkxuP3oCDi9vRi1lmTzOJyMEi8muMPPfEar1XmCQkCg12sD9QVBE1sIOltYkx2SK3BQQ/w640-h426/_P5A3676.jpg)
“Kipekee tuwashukuru wanawake wa Boko kwa wazo ambalo walikuwa nalo, wakachangishana wakatoa kwa moyo mkunjufu na kwa moyo wa kupenda na kuungana kwa pamoja na kuleta hii sadaka hapa muhimbili.” alisema na kuongeza kuwa urafiki kati ya watoto hao na umoja huo ulianza kwa kutoa huduma ya kujitoa matendo ya huruma kuanzia mwaka 2018 na imekuwa endelevu.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEirlKoXJcpOnoJJf_Y76PJirrWN1x7s_J342Ez5Ncf8lvnTo-ZqjlcM6Rh6IwFEEVpfU6GWwPKEeSbnYs7pZkZ3Df_IZKxApnJXldU6D17J8ZQcQDJVzsMi8fJ8vm-WVIPMs9RDJg8k4PVSoTa4KrlGPRnfpku3kqk3OwZxWRORlcFa_W67sB3jxBhhcg/w640-h426/_P5A3648.jpg)
Zuhura ametoa rai kwa wadau wengine kuwatembela na kutoa msaada wa hali na mali ambayo itasaidia kutoa huduma katika hospitali ya Taifa Muhimbili. katika kuiga mfano wa wanawake hao katika kujitoa kwa moyo kwani wamekuwa wakifanya hivyo kila mwaka.
“Hospitali kama hospitali tumebeba majukumu makubwa kuhakikisha kwamba kila rasilimali iliyopo inatumika kusaidia wagonjwa pamoja na wateja wote wanaokuja hospitali, hizi zawadi na misaada ya hali na mali tunayoipata tunaona njia mojawapo ambayo kwanza inatuweka karibu na jamii ambayo inatusaidia sisi kama wataalamu kutoa huduma kwa wateja wetu. Alisema.
Mkurugenzi huyo amewashukuru Wanawake wa KKKT usharika wa Boko na kusema kuwa msaada wao utaenda kuwapa faraja watoto wanaoendela na matibabu.
No comments:
Post a Comment