HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, June 25, 2022

SNURA, NEY, STAMINA, MC KINATA, CHEGE, MAUA SAMA WAITEKA TEMEKE, TAMASHA LA ZEGE DAY

 Na Khadija Kalili 

WASANII mbalimbali wa Kizazi Kipya  leo  Juni, 25,2022 wamefanikiwa kusimamisha Wialaya ya Temeke na viunga vya jirani jijini Dar es Salaam  kwa kuwakutanisha mashabiki mbalimbali kwenye tamasha la Kimataifa lililofahamika kama 'Zege Day' lililofanyika kwenye viwanja vya Mwembe Yanga

Tamasha Hilo ambalo lilinogeshwa na wasanii wenye mvuto katika miondoko mbalimbali ikiwemo singeli, bongo fleva na muziki wa dansi ni pamoja na Ney wa Mitegi, MC Kinata, Maua Sama, Snura Mushi na Mwanamuziki  mkongwe katika Tasnia ya muziki wa dansi Josse Mara.

Mbali ya wasanii hao wengine walio amsha hisia pindi walipopanda jukwaani ni pamoja na msanii  Stamina.

Huku wasanii wengine waliokonga nyoyo za mashabiki waliofika kwenye tamasha hilo la 'Zege Day' ni  pamoja na Dayoo, Micky Singer, Rasco Sambo, Lody Music, Sir Jay, Nedy Music, Kayumba, Mzee wa Bwax na Sholomwamba.

Akizungumza na waandishi wa Habari wakati tamasha hilo likiendelea mmoja wa viongozi wa Kampuni ya Clouds Media Group (MMG) Sebastian Maganga amelielezea tamasha hilo la Zege Day kwa kusema kuwa ni la Kimataifa na linafanyika  duniani kote  hivyo wao MMG wameratibu ikiwa ni katika kutambua na kuthamini mchango wa vijana wauza Chips kwa kuwarahisishia wakazi katika maeneo mbalimbali kupata chakula cha haraka.

"Sote tunajua kuwa  maisha ya kimjini yanaratiba ndefu na pana na hapo ndipo utamaduni wa Zege ulipoanzia  sisi kama Clouds tumejukita katika kutoa ajira  kwa vijana  ndipo tulipokaa na kukubalia kuja kufanya tamasha hili hapa Mwembe Yanga baada ya wapenda Zege lialia kupiga kura." Amesema Maganga.

Maganga ameongeza kuwa hakuna historia kamili inayoelezea ni wapi ilianzia Chips Zege lakini historia inasema kuwa watanzania wenye asili ya Bara  la Asia ndiyo walianza kuuza Chips maeneo ya Ilala Jijini Dar es Salaam na baadaye  chakula hicho kikajizolea umaarufu.

Aidha  Maganga amewashukuru wadhamini wa tamasha hilo ambao ni  kinywaji baridi cha Pepsi, The Kick na wazalishaji wa sausages.
Msanii wa Bongo Muvi na Muziki wa Kizazi kipya, Snura Mushi akitumbuiza katika tamasha la 'Zege Day' lililofanyika katika Viwanja vya Mwembe Yanga Temeke jijini Dar es Salaam leo Juni 25,2022.

Wasanii mbalimbali wa Muziki wa Kizazi kipya, Snura Mushi wakitumbuiza katika tamasha la 'Zege Day' lililofanyika katika Viwanja vya Mwembe Yanga Temeke jijini Dar es Salaam leo Juni 25,2022.Kampuni ya Clouds Media Group (MMG) Sebastian Maganga akinunua sausage wakati wa tamasha la 'Zege Day' lililofanyika katika Viwanja vya Mwembe Yanga Temeke jijini Dar es Salaam leo Juni 25,2022.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza katika tamasha la 'Zege Day' lililofanyika katika Viwanja vya Mwembe Yanga Temeke jijini Dar es Salaam leo Juni 25,2022.

Mtangazaji wa Clouds Tv, Sakina Lyoka akiwauzia Chips Zege wananchi waliohudhuria tamasha la 'Zege Day' lililofanyika katika Viwanja vya Mwembe Yanga Temeke jijini Dar es Salaam leo Juni 25,2022.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad