MWENGE
wa uhuru umezindua mradi wa kuhifadhi mazingira wa shule ya sekondari
Mgutwa iliyopo Kata ya Shambarai Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara wa
thamani ya shilingi 18,210,000.
Mkuu
wa shule ya sekondari Mgutwa Donald Lema akisoma taarifa ya mradi huo
kwa kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka huu Sahili Nyanzabara
Geraruma, amesema mradi huo una miti 2,150 iliyopandwa.
Mwalimu Lema amesema matarajio yao kwa mwaka huu ni kupanda miti ya matunda 350.
"Mradi
unaendelea vizuri na mafanikio yaliyopatikana ni kurejea kwa uoto
katika eneo la shule, upatikanaji wa kiviuli na kufanya shule kuwa na
mandhari nzuri zaidi ya kujisomea na upatikanaji wa matunda kwa ajili ya
wanafunzi," amesema mwalimu Lema.
Amesema
wanaamini mradi huo unachangia katika kupunguza kiasi cha hewa ya ukaa
kilichopo angani na kufanya eneo hilo kuwa mahalo pazuri zaidi kwa
maisha ya binadamu na viumbe wengine hai.
Amesema hiyo ina wanafunzi 131 wasichana 63 na wavulana 68 na walimu saba.
Amesema shule hiyo ilitembelewa na mwenge wa uhuru mwaka jana na kuona mradi huo upandaji miti na utunzaji mazingira.
"Lengo
la mradi ni kutunza mazingira ya shule na kuchangia juhudi za Serikali
katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi," amesema
mwalimu Lema.
Kiongozi wa
mbio za mwenge wa uhuru mwaka huu, Sahili Nyanzabara Geraruma
ameipongeza shule ya sekondari Mgutwa kwa kufanikisha mradi huo wa
kuhifadhi mazingira.
"Nawapongeza
kwa mradi mzuri ila mnapaswa kuutunza na hii miti tuliyoipanda mimi na
wakimbiza mwenge wenzangu wa kitaifa hakikisheni mnaitunza," amesema
Geraruma.
Mkuu wa Wilaya
ya Simanjiro Dk Suleiman Serera amesema ukiwa wilayani humo mwenge
utatembelea miradi sita ya thamani ya shilingi bilioni 1.3.
No comments:
Post a Comment