Na Mwandishi Wetu, Bukoba
Waendesha 
pikipiki maarufu kama bodaboda mkoani Kagera wamempongeza Rais wa 
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kupunguza 
gharama za mafuta.
Hatua ya kupunguza bei ya mafuta ilitokana na 
mtazamo chanya wa serikali wa kubana matumizi na kutoa ruzuku ya 
shilingi bilioni 100, jambo ambalo limesaidia kushuka kwa bei hapa 
nchini na kupunguza makali ya maisha.
Pongezi za bodaboda hao 
zimewasilishwa na Umoja wa Bodaboda wilayani Bukoba (UBOBU) ikiwa ni 
siku moja kabla ya Rais Samia kufika mkoani Kagera kwa ajili ya ziara ya
 kikazi ya siku tatu mkoani humo.
Mwenyekiti wa UBOBU, Mahamud 
Sued amesema ushushaji wa bei ya mafuta utalisaidia kundi kubwa la 
bodaboda kuweza kumudu gharama za maisha na kuepuka kujiingiza kwenye 
vitendo viovu.
"Ili kutambua ukubwa wa kundi hili kwa upande wa 
Manispaa ya Bukoba pekee kuna bodaboda 8,600 ndio maana tunaomba 
aendelee kutupunguzia gharama.
Ruzuku imetolewa kwa wakati muafaka na kutupa nahueni sisi ambao riziki zetu zinategemea sana bei ya mafuta."
Kabla
 ya kutolewa kwa ruzuku hiyo, kwa Bukoba mafuta yalikuwa yanauzwa 
shilingi 3,460 kwa Lita na Sasa yanauzwa shilingi 3,200 kwa lita kukiwa 
na punguzo ya shilingi 260 kwa lita.
"Pia bodaboda tunamuomba 
Rais Samia kurasimisha biashara ya bodaboda na kulitambua kama kundi 
maalum lenye uhitaji wa kuwekewa mazingira mazuri ya kibiashara kama 
inavyofanyika kwa wamachinga.
Kundi hili tupo watu wa kila aina, 
kuanzia waliomaliza darasa la saba au chini zaidi mpaka waliomaliza vyuo
 vikuu lakini wakakosa ajira. Wote tumejiingiza humu na kujiajiri 
kutafuta kipato ili kulea familia na wategemezi wetu kwa kufanya kazi 
halali ya uendeshaji wa bodaboda," alisema Sued.
Naye Naibu 
Waziri wa Nishati, Adv Steven Byabato alisema katika suala la kutoa 
ruzuku hiyo, Rais Samia ameupiga mwingi tena wa kimataifa kwa sababu 
mafuta hayajashuka bei bali Rais Samia ameshusha bei ya mafuta kwa 
kuweka hiyo fedha ya ruzuku.
Alisema kinachotakiwa ni kumuombea 
ili Rais Samia aweze kupambana kutafuta namna ya kushusha zaidi bei hiyo
 kwa kutafuta fedha nyingine zitakazosaidia punguza gharama kwa 
wananchi.
"Kwa sababu isingeweka hiyo ruzuku sasa hivi Bukoba tungekuwa tunanunua mafuta 3700 au 3800 pengine hata na zaidi.
Na
 bei hiyo inaendelea kupanda duniani kwa sababu upatikanaji wa bidhaa 
hiyo ni mdogo kuliko uhitaji wake ambao ni mkubwa," alisema Byabato.
Byabato
 alisema kwa Tanzania mafuta hayashuka bali kutokana na huruma ya Rais 
inayotokana na umama ameamua kuweka fedha hizo ili kushusha bei kwa 
lengo la kupunguza ukali wa maisha.
"Katika kitu ambacho Rais 
Samia ametusaidia ni kuweka shilingi bilioni 100, na ninawaahidi huko 
tunakoelekea ni kuzuri zaidi," alisisitiza.
Wednesday, June 8, 2022
 
BODA BODA BUKOBA WAMPONGEZA RAIS SAMIA,WAOMBA WARASIMISHWE
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment