HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, June 1, 2022

ATCL KUANZA TENA SAFARI CHINA MWEZI JUNI 2022

 

SERIKALIimesema kuanzia mwezi Juni 2022 Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) limeruhusiwa kusafirisha tena abiria nchini China.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb) jana jioni wakati alipokuwa akijibu hoja za wabunge kuhusu mkakati wa Wizara katika kukuza na kuetekeleza Diplomasia ya Uchumi.

“Lakini pia Mhe. Naibu Spika kuna habari njema, na Habari ambayo nimeipokea wiki hii ni kwamba kuanzia Juni mwaka huu Shirika letu la ndege limeruhusiwa kuanza tena safari zake kubeba abiria kwenda China,” alisema Balozi Mbarouk.

Machi 2020, Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) lilitangaza kusitisha safari za ndege kuelekea China kutokana na kuwapo kwa ugonjwa wa virusi vya Corona.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad