*Aeleza sababu zilizomsukuma, ampongeza na kumshukuru Rais Samia
*Nape amtaja jinsi alivyomsaidia safari yake ya siasa kutwaa jimbo
*Shaka aongoza mapokezi yake ya kishindo na kumkabidhi kadi
Na Mwandishi Wetu, Lindi
ALIYEKUWA
mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi Mkuu
wa mwaka 2015, kupitia Chama cha ACT Wazalendo ameeleza sababu
zilizomfanya arejee CCM ikiwemo kuondoka kwa sababu ambayo ilimfanya
atimkie upinzani.
Aidha amefungunguka jinsi alivyoumia kutokana
na uamuzi wa kumwondolea uanachama wa CCM, Chama alichokulia huku
akiahidi kufia ndani ya CCM.
Membe ambaye amewahi kuwa Waziri wa
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa katika Serikali ya Awamu ya
Nne, alirejea rasmi CCM jana kupokelewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya
Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka, katika mkutano
wa Hadhara wa Mbunge wa Mtama, Nape Nape Nnauye uliofanyika katika Kata
ya Chipomda, Jimbo la Mtama mkoani Lindi, alisema kurejea kwake
kunatokana na dhamira ya kukitumikia Chama hadi kufa.
Akizungumza
katika mkutano huo, katika Kijiji cha Rondo, alisema Machi 30 hadi
Aprili 1, mwaka huu aliitwa Dodoma, kwenye Mkutano wa Kamati Kuu ya
Maadili na Mkutano Mkuu wa Halmashauri Kuu, alipewa nafasi na Mwenyekiti
wa CCM Taifa kuzungumza na wana CCM.
“Mama yetu, Rais wetu na
Mwenyekiti wetu wa CCM Taifa alinipa nafasi ya kuzungumza na wajumbe wa
kamati kuu ya Chama Taifa. Nashukuru kwa kupewa nafasi ile na wajumbe
waliliridhia kwa kauli moja nirejee CCM.
“Nimerejea CCM kwa
sababu kuu mbili, sababu ya kwanza nilishauriwa na viongozi wa dini
zote, nilishauriwa na viongozi wa CCM ngazi ya Wilaya na Mkoa,
nilishauriwa na marafiki zangu wote nirejee CCM, nilishauriwa na wana
CCM.
“Kutokana na ushauri wote huo sikuwa na namna nyingine zaidi
ya kutii, nimekubaliana na ushauri wa wote waliosema nirudi CCM na sasa
nimerudi CCM,” amesema Membe wakati akitangaza kurejea tena kwenye
Chama.
Amesema sababu ya pili ya kurudi kwenye Chama hicho
inatokana na dhamira yake ya kukitumikia Chama Cha Mapinduzi hadi
atakapokwenda kaburini. “Nilipoondolewa CCM nilisikitika sana,
nilisonekana sana, na ninyi wananchi msikitika, mlisononekana.
“Sababu
ambazo zilinifanya niondoke CCM haziko tena, narudi sababu
zilizoniondoa CCM haziko tena. Nimerudi, namshukuru Mwenyekiti wa CCM na
wajumbe wa Kamati Kuu kunirudisha. Nimerudi kwenye Chama ambacho
nimezaliwa na kukulia, chama ambacho kimenisomesha.
“Hivyo
niahidi sitaondoka tena, nitabakia CCM hadi mwisho wa uhai wangu.
Kurudi kwangu CCM nitaendelea kukitumikia Chama changu na sasa
nitaendelea kushirikiana na Mbunge wangu Nape Nnauye. Mwaka 2015
nilisema nitawaletea Nape na kweli nilimleta, hivyo sasa Mtama mtakuwa
na wabunge wawili, Mbunge wetu Nape na mimi mbunge wa chini chini.”
NAPE
Kwa
upande wake Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari,
Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye alisema baada ya Membe
kuondoka kwenye Chama wananchi wengi walichukia, lakini aliwaomba
wasichukie kwani kuna siku moja atarejea.
“Leo mwenyezi Mungu
ameturudishia faraja la Londo, ameturejeshea furaha Chiponda. Mtama ni
wastaarabu na hatuna shida tena, tuna imani kubwa na Membe, alinikabidhi
kijiti na kuvaa viatu vyake, kulikuwa na mambo yaliyokwama huku nyuma
kwa sababu za kisiasa, lakini Mama Samia amekuja ameziondoa,” alisema.
Aidha,
alitumia nafasi hiyo kuwataka wananchi wa Mtama kushikamana, fitina
ambazo ziliingia kati zimekwisha. “Membe amenipigania katika mambo
mengi, nilipotaka ubunge Ubungo baada ya kuonekana fitna zimeingia
katikati Membe aliamua kuchora ramani.
“Ndio maana safari yangu
ya ubunge imekuwa nyepesi. Kaka Membe amenipigania sana na bahati nzuri
amerudi CCM. Niseme tu Mungu ameamua ugomvi,” alsema.
SHAKA AMKABIDHI KADI
Akizungumza
katika mkutano huo, Shaka alisema Memembe amerejedushwa katika Chama
baada ya kufuatwa kwa utaratibu ikiwemo kujadiliwa na tawi lake kisha na
vikao vya juu.
Shaka alisema Membe na wanachama wengine zaidi ya
1670 waliovuliwa uanachama ambao wamejadiliwa katika vikao na
kurejeshewa uanachama, sasa wanaweza kukabidhiwa kadi zao katika matawi
yao.
Shaka alisema kurejea kwa Membe ndani ya CCM kuendelee kuwa
chachu ya kudumisha umoja na mshikamano hususan kwa wanaccm wa Jimbo la
Mtama.
No comments:
Post a Comment