Wizara
ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum imekubaliana
na Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu (UNFPA) kushirikiana
kutafuta namna na mbinu bora zitakazoiwezesha Tanzania kuzingatia
misingi ya Usawa wa kijinsia.
Makubaliano hayo yamefikiwa
(Aprili 06, 2022) Jijini Dar Es Salaam wakati wa Kikao kati ya Wizara
na Wadau wa Maendeleo kuhusu masuala ya Usawa wa Kijinsia kutoka
UNFPA.
Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Zainab Chaula amesema, Tanzania
itahakikisha masuala yote kuhusu usawa wa kijinsia yanazingatiwa kwa
kuwapa fursa wanawake katika Nyanja mbalimbali zikiwemo za uongozi na
kiuchumi.
" Tunaongozwa na Miongozo mbalimbali ikiwemo Dira ya
Taifa …..na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) 2020-2025, hivyo,
niwaombe tu, tuzingatie haya kwenye mipango yetu Shabaha ni twende
pamoja kwa matokeo chanya na ya haraka" alisema Dkt. Chaula
Amesema
jukumu kubwa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ni kushirikiana na
Serikali kutatua changamoto zinazoikabili jamii ikiwemo ukatili wa
kijinsia unaozidi kushamiri.
" Tunasikia kila siku ukatili,
mauaji sasa tushirikiane tuweke nguvu ya pamoja, tuwekeze katika elimu
kwa jamii, hii itasaidia kuondokana na vitendo vya ukatili " alisema
Dkt. Chaula
Akichangia mada wakati wa kikao hicho Naibu Katibu
Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum,
Amon Mpanju amesema, Wizara itaendelea kushirikiana na wadau kutafuta
suluhu ya ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto.
Kwa upande wake
Mshauri wa masuala ya Kijinsia kutoka UNFPA Maja Hansen amesema Shirika
hilo liko tayari kushirikiana na Wizara katika utekelezaji wa Mipango
mbalimbali ikiwemo Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya
Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) 2017/2018-2021/2022.
Mkutano kati
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum na
UNFPA ni muendelezo wa vikao vya majadiliano na wadau mbalimbali kwa
lengo la kutatua changamoto za jamii.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Amon Mpanju akichangia Jambo wakati wa kikao cha Wizara na Wawakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu (UNFPA) kwenye Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar Es Salaam tarehe 06/04/2022.
Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt Zainab Chaula akizungumza na Wawakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu (UNFPA) katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar Es Salaam tarehe 06/04/2022.Mshauri wa masuala ya Kijinsia kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu (UNFPA) Maja Hansen akimueleza Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Zainab Chaula vipaumbele vya Shirika hilo alipotembelea ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam tarehe 06/04/2022. Baadhi ya Wakurugenzi na Maafisa wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum katika kikao na Wawakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu (UNFPA) katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam tarehe 06/04/2022. Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Zainab Chaula katika picha ya pamoja na Wawakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu (UNFPA) mara baada ya kikao kati ya Wizara na Shirika hilo kilichofanyika Jijini DSM (kushoto/Kulia)
Picha/Habari: Atley Kuni na Raymond Mushumbusi, WMJJWM
No comments:
Post a Comment