Waislamu
na wanajamii kwa ujumla wametakiwa kuutumia mwezi Mtukufu wa Ramadhani
kubadili tabia kwa kutenda yaliyo mema na kuyaendeleza hata baada ya
kumalizika mfungo.
Rai hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya
Wakurugenzi wa kampuni GF Truck & Equipments LTD, Mehboob Karmali
mara baada ya kufuturisha wadau mbali mbali na wafanyakazi wa kampuni
hiyo .
Alisema mara nyingi mwezi huo umekuwa ukileta utulivu
katika jamii, “Haijalishi ni kijana, mzee, Muislamu na asiyekuwa
mwislamu, ilimradi wengi hutulia na kuuheshimu, hivyo ni vema kuendeleza
yale mema hata katika nyakati nyingine ili jamii iwe salama.
“Kipindi
hiki pia ni vema kuwapa wahitaji sadaka kwa kile kidogo
tutakachojaaliwa kwa sababu tunazidiana “alisema Karmali.Kwa upande wa
mgeni mualikwa katika Iftari hiyo, Sheikh wa msikiti wa Khoja Shia
Ishnashri Jamaat ya nchini Uingereza, Syed Ali Raza Rizvi aliwasihi
Waislamu hususani vijana kudumisha amani na upendo baina yao.
Pia
alitumia fursa hiyo kuwaasa wafanyakazi wa kampuni hiyo kufanya kazi
huku wakimtanguliza Mungu ili wanapofanya maamuzi yoyote yawe kwa faida
ya kazi yao na Taifa kwa ujumla.
“Ukimtanguliza Mungu katika kila
jambo lazima utafanikiwa, ila ukiwajali wengine na kuwahurumia utafanya
maamuzi ya busara siku zote, hivyo tuyazingatie haya ili kufikia
mafanikio tunayoyakusudia”alisema Raza Rizvi.
Hii ni kawaida
kampuni ya GF Trucks & Equipemnts LTD, kujumuia na wafanyakazi wake
na wadau katika matukio mbalimbali ikiwamo kufuturisha pamoja na kutoa
misaada kwa yatima na wasiojiweza.
Kampuni hiyo inajishughulisha na uuzaji wa magari makubwa(trucks) na mitambo ya kutengenezea barabara.
Mkurugenzi wa kampuni ya Gf Truks & Equipment’s Ltd, Imran Karmali akimwangalia mfanyaklazi wa kampuni, Isack Shehemba hiyo aliye jishindia Redio (saboufa) wakati wa hafla ya Iftari iliyoandaliwa na kampuni hiyo iliyofanyika jijini Dar SalaamMwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa kampuni ya Gf Truks & Equipments Ltd, Mehboob Karmali (kushoto)akimkaribisha Shekh wa mskiti wa Khoja Shia Ishnashri Jamaat ya nchini Uingereza Shekh, Syed Ali Raza Rizvi wakati wa hafla ya Iftari iliyoandaliwa na kampuni hiyo iliyofanyika jijini Dar Salaam.
Baadhi ya wadau na wafanyakazi wakichukua chakula
Shekh wa mskiti wa Khoja Shia Ishnashri Jamaat ya nchini Uingereza Shekh, Syed Ali Raza Rizvi akiangalia zawadi ya Tasbihi bada ya kupewa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa kampuni ya Gf Truks & Equipments Ltd, Mehboob Karmali wakati wa hafla ya Iftari iliyoandaliwa na kampuni hiyo iliyofanyika jijini Dar Salaam.Kushoto ni All Jawad Karmal
Wageni waalikwa wakiwa katika Picha ya pamoja
No comments:
Post a Comment