Na Mwandishi Wetu
UBALOZI
wa Tanzania nchini Ufaransa kwa kushirikiana na taasisi ya kuendeleza
sekta ya horticulture Tanzania (TAHA), umefanya Mkutano wa kutangaza
fursa za bidhaa za matunda na mbogamboga (horticultural products) za
Tanzania ili kuingia kwenye soko la nchi za Ulaya hususan Ufaransa.
Mkutano
huo ulifanyika katika ukumbi wa Ubalozi na kuhudhuriwa na wafanya
biashara wakubwa wa sekta hiyo. Katika mkutano huo, Mtendaji Mkuu wa
(TAHA), Dkt Jacqueline Mkindi alielezea kuhusu ubora wa mazao kutoka
Tanzania ambayo yanaweza kuuzwa katika soko la Ufaransa na la ulaya.
Katika
taarifa yake, alisema kwamba tayari bidhaa nyingi zimeshaanza kuuzwa
katika masoko mengi ya nchi za Ulaya na sasa anataka mazao hayo kuingia
kwa wingi na kupata masoko nchini Ufaransa.
TAHA ilitia saini
Mkataba wa Makubaliano (MOU) na kampuni ya Laparra ya Ufaransa, ambao
ni waingizaji na wauzaji wakubwa wa mazao ya horticulture katika masoko
ya Ufaransa. Makubaliano hayo yanalenga katika kutangaza na kuuza bidhaa
(promotion and branding), katika masoko ya ndani na nje ya Ufaransa
ikiwa ni mkakati wa kuendeleza sekta hiyo nchini Tanzania.
Kabla
ya mkutano huo, Dkt Jacqueline Mkindi akiambatana na Mhe. Balozi Samwel
W. Shekukindo, Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa walipata fursa ya
kutembelea soko la kimataifa la Rungis (Soko kubwa kuliko yote la mazao
ya kilimo katika bara la Ulaya).
No comments:
Post a Comment