Na Khadija Kalili , Kibaha
Mkuu
wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amemwagia sifa Rais wa Jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ameonyesha nafasi na
uwezo wa Mwanamke duniani kutokana na uwezo wake mkubwa ameonyesha
katika kuwajibika.
Amesema hayo wakati akizindua siku ya Wanawake
duniani kimkoa katika viwanja vya Mailimoja mjini Kibaha na kuhudhuriwa
na akinamama kutoka mkoa mzima wa Pwani.
Alisema hata wale ambao
walikua na mashaka juu ya uongozi wa mwanamke kwa sasa kutokana na
namna anavyoupiga mwingi hawana la kusema hivyo wanawake wote tembeeni
kifua mbele kwani tunaye Kiongozi imara na madhubuti mwenye jinsia ya
kike.
Hata hivyo Mkuu huyo wa mkoa amewataka wadau wote
wanaojishughulisha na masuala ya malezi ya watoto wa kike wakajifunze
kwenye shirika lisilokuwa la kiserikali la Room to read ambalo
linamuhudumia mtoto wa kike katika shule za msingi na sekondari za
serikali kwa kutoa mafunzo ya stadi za maisha.
Alisema jinsi
shirika hilo la Room to read linavyotoa ushauri, msaada wa vifaa na
ushirikishwaji wa familia shule na jamii sambamba, elimu ya fedha na
ujasiriamali na masuala ya usomaji na maktaba ni mbinu madhubuti katika
kukusaidia moto wa kike na mwanamke kwa ujumla kujilinda hadi afikie
malengo yake.
Aidha Alhaji Kunenge amewataka wanawake
wajasiriamali kujituma zaidi Ili kuweza kujikomboa kiuchumi kwa kuleta
maendeleo ndani ya familia na Taifa kwa ujumla.
RC Kunenge
amesema haya leo Machi mbili katika viwanja vya Maili Moja Wilayani
Kibaha alipokuwa akizindua sherehe za kuelekea siku ya Wanawake
Duniani ambayo itaadhimishwa duniani kote ifikapo Machi nane ambapo kwa
Mkoa wa Pwani maadhimisho haya yatafanyika kimkoa katika Halmashauri ya
Chalinze huku kauli mbiu ya mwaka huu inasema 'Haki na Usawa kwa
maendeleo Endelevu'.
Mkuu huyo wa Mkoa amewaahidi wajasiriamali
hao kuwa atakutana nao Ili waweze kujadili masuala mbalimbali yanayo
wahusu na siku hiyo atajaa nao kama Alhaji Kunenge huku akisisitiza kuwa
wawe huru siku hiyo katika kuzungumza nae kwa kinaga ubaga.
"Tutakaa
nawenzangu tuangalie namna ya kuweza kutoa mkopo wenye tija
utakaomwezesha mkopaji kufanya jambo la maana pia tutawasaidia kuwapa
mafunzo na miongozo Ili wakopaji waweze kukopeshwa wakishafanikiwa
waweze kukopeshwa wengine hili liko ndani ya uwezo wetu nitalijadili na
Kamati yangu"alisemaKunenge.
Kila kikundi tutawafikia hakuna
kundi au mtu atakayeachwa tutajitahidi tufungue fursa zaidi kwani njia
ya kuwasaidia nyie ni kutoa fursa zaidi za kibiashara ,tuzingtie sheria
na tutumie fursa.
"Tuhakikishe sisi sote tunashiriki katika sensa
ya watu na makazi tujitokeze tushiriki vizuri na tupate chanjo za
ugonjwa wa UVICO 19 takwimu zinaonyesha katika nchi yetu wale ambao
hawajapata chanjo ndiyo wanaopata madhara zaidi" alisema Kunenge.
Katika
sherehe hizo zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Kamati ya
Ulinzi na Usala ya Mkoa wa Pwani wengine ni pamoja na Mwenyekiti wa
Umoja wa Wanawake Mkoa wa Pwani (UWT)Farida Mgomi ambaye alisema kuwa
uzinduzi huu utaambatana na kufanyika maonyesho ya bidhaa mbalimbali za
wajasiriamali wa Wilaya Kibaha huku akitoa wito kwa wakazi wa Wilayani
hapa kujitokeza katika kuwaunga mkono.
"Alisema kuwa baada ya
uzinduzi huu Machi sita kutafanyika usiku Maalumu utakaofahamika kwa
jina la Usiku wa wa Mwanamke wa Pwani ambapo kutafanyika mambo
mbalimbali hasa kujua Mila na desturi za Mkoa waPwani' alisema
Mwenyekiti huyo.
Mbunge wa Viti Maalum wa Mkoa wa Pwani Subira
Mgalu ametoa pongezi kubwa kwa Wilaya na Mkoa kuandaa sherehe hizi
ambazo kilele chake ni Machi nane .
Mkuu wa Wilaya Sara Msafiri
alisema kuwa mwaka huu Wilaya imejipanga hivyo wataendelea kutoa
misaada mbalimbali ikiwemo kwenda kutembelea waginjwa katika Hospitali
ya Ocean Road, gereza la Mkuza ambapo baadhi ya wanawake kutokaWilayani
hapa watakwenda kutoa misaada.
"Tumejipanga kuwajengea uwezo
kina mama kwa kuwapa mafunzo Maalumu Ili waweze kupanda madaraja katika
biashara zao mwisho napenda kywashukuru wadhamini wetu ambao ni NMB,
TRA, OSHA,TARURA,ROOM TO READ,TANESCO,DAWASA,TAKUKURU,.
Bendi ya
muziki wa dansi ya Ruvu JKT ilitumbuiza sambamba na wasanii wengine kama
Msaga Sumu, Yuda wote walinogesha uzinduzi huo
Maadhimisho ya siku ya Wanawake duniani ilianzishwa mwaka 1908 na kwa sasa inaadhimishwa mwaka 101.
No comments:
Post a Comment