
WAZIRI
 MKUU Kassim Majaliwa ametangaza uamuzi wa Serikali wa kuondoa tozo 42 
kati ya 47 ambazo walikuwa wanatozwa wakulima wa kahawa wa Mkoa wa 
Kagera hadi kufikia tozo 5 tu ambazo itakuwa ni jumla ya Shilingi 267 
kwa kila kilo ya kahawa, kutoka Shilingi 830 za awali. 
Waziri 
Mkuu ametoa maamuzi hayo kufuatia tume maalum aliyoiunda ili kupitia 
utaratibu na mfumo wa uendeshaji wa vyama vya Ushirika wa zao la kahawa 
Mkoani Kagera. 
Mheshimiwa Majaliwa amewaagiza viongozi wa vyama 
vya Ushirika, wasimamie vyama vyao kwa uaminifu na weledi ili vilete 
tija kwa wakulima. 
Pia, Mheshimiwa Majaliwa amewata viongozi wa 
vyama vikuu vya ushirika kuacha tabia ya kukopa pesa benki kwa ajili ya 
kununua kahawa kwa wakulima. 
Waziri Mkuu ameyatoa maagizo hayo 
leo (Jumanne, Machi 29, 2022) Wakati alipoendesha Mkutano Maalum wa 
Wadau wa zao la kahawa mkoani Kagera uliofanyika wilayani Karagwe Mkoa 
wa Kagera. 
Amesema kuanzia sasa mauzo ya kahawa katika Mkoa wa 
Kagera yatafanyika kwa njia ya mnada. “Mnada huo utafanyika kwenye ngazi
 ya vyama vya msingi.” 
Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema 
baadhi ya vyama vya ushirika vimekuwa vikiwaumiza wakulima wa kahawa kwa
 kuwaongezea tozo zisizokuwa na tija. 
Amesema jambo hilo 
linafanyiwa kazi kwani wakulima wa kahawa mkoani Kagera wamekuwa wakilia
 na tozo kubwa zaidi ya 47 na bado wamekuwa wakicheleweshewa malipo. 
Waziri
 huyo amemuagiza Mkurugenzi wa Bodi ya Kahawa kugawa miche ya kutosha ya
 kahawa kwa wakulima ili ilete tija na kuwaongezea kipato. 
Amesema
 ili kuhakikisha maafisa ugani wanatekeleza majukumu yao ipasavyo Wizara
 imeandaa utaratibu wa kutoa usafiri pamoja na vifaa vya kupimia udongo.
 
Awali, Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Prof. Faustin Kamuzora 
alisema katika msimu wa kilimo wa mwaka 2021/2022 mkoa ulizalisha jumla 
ya tani 52,000 za kahawa ya maganda iliyokuwa na thamani ya sh. bilioni 
69. 
“Bei ya kahawa imeendelea kuimarika kwani katika msimu huu 
wakulimwa walilipwa shilingi elfu 1,300 kwa kilo moja ya kahawa ya 
maganda na Shilingi elfu 3,300 kwa kilo moja ya kahawa hai (Organic 
cofee).” 
Naye, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Innocent 
Bashungwa alisema kutokana na usimamizi mzuri wa Serikali ya awamu ya 
sita katika zao la kahawa, tayari wakulima wemeanza kuona manufaa kwani 
bei ya zao hilo imepanda. 
Kwa Upande wake, Mwenyekiti wa Tume 
Maalumu ya kuchunguza mwenendo wa zao hilo. Dkt. Fabian Magawa Madele, 
alisema katika uchunguzi waligundua ubadhirifu wa zaidi ya shilingi 
bilioni saba ambazo zilitumika nje ya utaratibu wa vyama vya Ushirika.
Wednesday, March 30, 2022
 
SERIKALI YAFUTA TOZO 42 ZAO LA KAHAWA-MAJALIWA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment