Na Amiri Kilagalila,Njombe
Mwenyekiti
wa jumuiya ya wanawake Tanzania (UWT) wilaya ya Njombe Betreace
Malekela,ametoa wito kwa wanawake kupendana na kusemeana vizuri ili
waweze kufanikiwa na kukuza uchumi wao.
Ametoa wito huo wakati
akizungumza na baadhi ya wanawake mjini Njombe walioukutana katika hafla
fupi iliyofanyika katika ukiumbi wa Miriam ili kuhamasishana na kupeana
faraja katika majukumu yao.
“Kila aliyempenda jirani yake
amefanikiwa,msichongeane,msichukiane niwaombe mnapokuwepo kazini
mpendane na utamani sana mwenzako apande katika nafasi.Ni vizuri sana
kusemeana kwenye kazi naamini utafanikiwa”alisema Betreace Malekela
Iren
Nyambo ni muunadaaji wa tukio hilo lililowakutanisha wanawake,amesema
lengo kubwa ni kila mmoja kujifunza na kutengeneza mahusiano ili
kuyafikia mafanikio.
“Tumekutana wawake wa aina tofauti wakiwemo
wajasiriamlai na watumishi wengine kwenye makampuni na taasisi mbali
mbali za serikali na zisizo za kiserikali kwa kuwa tukikaa pamoja na
kujifunza tutafanya vitu vikubwa sana”alisema Iren Nyambo.
Sandra
Msigwa ni mmoja wa washiriki wa tukio hilo la wanawake ambaye pia
ameweza kutoa maada katika tukio hilo amesema mikusanyiko hiyo imekuwa
ikileta manufaa makubwa kwao na kutoa wito wanawake kujiamini,kujipenda
na kujijari.
“Ninaendelea kuhamasisha wanawake
kujiamini,kujipenda na kujijari kwasababu mtu ukijiamini itakuwa rahisi
sana kuchangamkia fursa”alisema Sandra.
No comments:
Post a Comment