Kampuni
ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania kupitia kampeini maalum ya
kusaidia jamii kwa kipindi hiki cha msimu wa sikukuu ambayo inalenga
kuwanufaisha watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, leo imetoa msaada
wa vyakula kwa kituo cha watoto yatima cha Mtakatifu Yohana Paul cha
mkoani Katavi. Kampeini hiyo ya wafanye watabasamu, ilizinduliwa
mwishoni mwa mwaka jana na inalenga kunufaisha vituo 12 vya watoto
yatima hapa nchini.
Akiongea
mara baada ya kutoa msaada huo kwa kituo hicho cha Mtakatifu Yohana
Paul, Mkuu wa Mauzo Airtel Mkoa wa Katavi Bartholomew Masatu alisema
muda mrefu imekuwa na utamanduni wa kusaidia jamii na kwa kipindi cha
msimu wa sikukuu, kampuni iliona ni vyema ikatumia kwa kusherehekea na
watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.
Leo
ni siku yenye furaha sana kwetu zote kwani mayatima ni sehemu ya Jamii
yetu na ni muhimu kuwapa upendo pamoja na kuwafariji. Hiki ambacho
tumekuja kutoa leo hapa ni kidogo lakini nina uhakika kitagusa mioyo
yenu lakini zaidi ni kujua tuko pamoja nanyi na tunawajali sana, alisema
Masatu.
Tunayo
furaha kuweza kuwafikia watoto hawa ambao wako kwenye kituo hiki na
dhamira yetu ni kuendelea kugusa maisha ya watoto wanaoishi kwenye
mazingira mangumu na kuwafanya wajisikia kuwa sehemu ya familia ya
Airtel, aliongeza Masatu.
Kwa
upande wake, Mama Mkuu wa kituo cha Mtakatifu Yohana Paul Sista Rose
Sungura alisema ni furaha kwa kampuni kubwa ya Airtel kuguzwa na maisha
ya watoto wanaoishi kwenye kituo hiki na hatimaye kuja kutoa msaada na
kutuunga mkono.
Najua
kuna vituo vingi vya mayatima hapa nchini kama sisi hapa. Kuamua kuja
kuwa na sisi ni Baraka kubwa kwetu. Nachukua fursa hii kuwapongeza wote
kwa kile mlichotoa ambacho mnaweza kudhani ni kidogo lakini kinaleta
matumaini makubwa kwetu na hasa kwa hawa watoto. Naomba kuwakaribisha
tena hapa na sio lazima kuja kutoa msaada, lakini mnapokuja kujumuika na
hawa watoto wanapata faraja kubwa na kujisikia kama sehemu ya Jamii
kwani wengi wao hapa hawajawahi kuona Wazazi wao, alisema Sungura.
Mkuu
wa Mauzo wa Airtel Tanzania kwa Mkoa wa Katavi Bartholomew Masatu
(kushoto) akimkabidhi Mama Mkuu wa Kituo cha Mtakatifu Yohane Paul cha
mkoani Katavi Rose Sungura (katikati) baadhi ya msaada uliotolewa na
kampuni ya Airtel Tanzania ikiwa ni ishara ya kuonesha upendo kwa
kipindi hiki cha msimu wa sikukuu. Kulia ni Afisa Maendeleo ya Jamii
Mkoa wa Katavi Anna Shumbi.
No comments:
Post a Comment